
NAMNA anavyojua kutekeleza majukumu yake kwa ufanisi, akiwahimiza wenzake kukaba mpaka kivuli, huku akionyesha mfano, imemfanya beki wa kimataifa wa mabingwa wapya wa Kombe la Kagame, Azam FC , Serge Pascal Wawa kubatizwa jina la Waziri wa Ulinzi.
Jina na cheo hicho si cha kwanza kusikika hapa
nchini, miaka kadhaa nyuma aliwahi kupewa Hamis Yusuf beki aliyewahi
kung’ara na timu kadhaa ikiwamo Yanga na African Lyon kwa jinsi staili
yake ya uchezaji ilivyokuwa kikwazo kwa washambuliaji wasumbufu.
Muulize Amissi Tambwe au Donald Ngoma wa Yanga
watakufafanulia vizuri namna beki huyo wa kati ya Azam alivyokuwa
akikaba mpaka vivuli vyao kiasi cha kushindwa kufurukuta na kuishuhudia
timu yao ikiaga mashindano ya Kombe la Kagame yaliyomaliza juzi
Jumapili.
Wawa anafahamu kitu gani kilichomleta Tanzania,
thamani yake kwa Azam imelipa kwa kazi nzuri ambayo amekuwa akiifanya
tangu atue akitokea El Marreikh ya Sudan kuanzia kwenye Ligi Kuu mpaka
kwenye Kombe la Kagame.
Ndiyo maana haikuwa ajabu katika michezo sita
ambayo mchezaji huyo aliiwakilisha Azam kwenye michuano ya Kagame
kushinda tuzo ya mchezaji bora wa mechi mara tatu kabla ya kuibuka kuwa
Mchezaji Bora wa michuano hiyo.
Mwanaspoti ilifanya naye mahojiano maalumu na kueleza mambo kadhaa ikiwamo kwa nini anaitwa Waziri wa Ulinzi wa Azam?
Ubora
Wawa anakiri kupachikwa jina hilo na wachezaji
wenzake pengine kutokana na ubora wake wa kucheza kwa bidii, kujituma na
kuisaidia timu na kuhakikisha hakuna straika anayeleta tabu kwa makipa
wao.
Anasema licha ya changamoto kubwa anazokutana nazo
kama mchezaji, bado anajitahidi kuhakikisha Azam inakuwa ikifanya vema
katika kila mchezo akishirikiana na wenzake kwa kutambua kuwa bila
ushirikiano ni vigumu yeye kung’ara pekee yake.
RSS Feed
Twitter
5:35 AM
Unknown
Posted in
0 comments:
Post a Comment