
KOCHA mkuu wa Simba, Dylan Kerr, ana changamoto kubwa visiwani hapa, kazi yake si rahisi hata kidogo.
Licha ya timu yake kushinda mechi tatu za awali za kirafiki, bado ana kazi kubwa kuhakikisha anapata timu bora zaidi.
Simba ilicheza mechi za kirafiki dhidi ya Kombaini
ya Zanzibar na kushinda 2-1, ikaifunga Braxeria 4-0 na kisha kuifunga
Polisi Zanzibar mabao 2-0.
Hata hivyo licha ya matokeo hayo kuna mambo bado
yanampasua kichwa kocha Kerr. Kocha huyo raia wa Uingereza pamoja na
yule wa viungo, Mserbia Dusan Momcilovic, wana kibarua kizito
kuhakikisha kuwa timu hiyo inakuwa bora kuliko wapinzani wao wakubwa
Yanga na Azam.
Mwanaspoti ambayo imeweka kambi pamoja na timu
hiyo visiwani hapa inakuletea mambo ambayo ni changamoto kubwa kwa kocha
huyo pamoja na wasaidizi wake.
Uwiano wa kikosi
Kwa bahati mbaya Simba ina viungo wengi kuliko
wachezaji wa idara nyingine. Timu hiyo ina viungo zaidi ya 10. Ina Jonas
Mkude, Mwinyi Kazimoto, Said Ndemla, Abdi Banda, Peter Mwalyanzi,
Michael Mgimwa, Awadh Juma, Mbarouk Yusuf, Simon Sserunkuma na kiungo
anayejaribiwa Justice Mujabvi.
Wingi huu wa viungo unamfanya Kerr kukosa uwiano
sahihi wa kikosi chake. Uchaguzi mpana alionao katika safu ya kiungo
haupo katika nafasi nyingine. Hapa ana kazi kubwa ya kufanya ili
kuhakikisha anapata kikosi chenye uwiano mpana.
Kusuka kombinesheni
Simba sasa ina wachezaji wengi wazuri, lakini bado
wameshindwa kucheza kwa uelewano mkubwa. Hii inamaanisha kuwa Kerr ana
kazi ngumu ya kusuka kombinesheni mbalimbali katika timu yake.
0 comments:
Post a Comment