
KIUNGO Mwinyi Kazimoto amekubali kurudi Simba kwa dola 25,000 sawa na Sh50 milioni ambapo dau hilo ni zaidi ya mshahara wa mwezi wa Rais wa Guinea, Alpha Conde, ambaye analipwa dola 22,000 kwa mwezi.
Kwa mujibu wa uchambuzi wa mtandao wa African
Review, Rais huyo ni miongoni mwa marais kumi wa Afrika wanaolipwa
mishahara midogo.
Kwa Afrika Mashariki Rais wa Uganda, Yoweri
Museveni ndiye anayelipwa kidogo zaidi ambapo mshahara wake kwa mwezi ni
dola 13,000(Sh26 mil), Rais wa Kenya Uhuru Kenyatta analipwa dola
132,000(Sh268 mil).
Uchunguzi wa mtandao huo umedai kwamba Rais wa
Rwanda, Paul Kagame dola 85,000 (Sh173 mil) na Rais Jakaya Kikwette
analipwa dola 192,000 (Sh390 milioni), Kikwette ndiye Rais anayelipwa
zaidi Afrika Mashariki.
Turudi kwa Kazimoto. Mshahara wa Kazimoto kwa
mwezi ni analipwa Sh2 milioni ambapo amesaini mkataba wa miaka miwili.
Kwa maana hiyo, Kazimoto ataikomba Simba jumla ya Sh 98 milioni kwa
miaka miwili ambapo fedha ya usajili ni Sh 50 milioni wakati mshahara
kwa miaka miwili ni Sh 48 milioni.
Habari kutoka ndani ya Simba, zinasema kuwa kiungo
huyo ambaye pia alikuwa akiwaniwa na Azam FC atajiunga na wenzake
keshokutwa Alhamisi katika kambi yao iliyopo visiwani Zanzibar ikiwa ni
pamoja na straika wao mpya, Laudit Mavugo aliyedaiwa kuwa ataingia leo
Jumanne au kesho Jumatano akitokea kwao Burundi.
Dili la kumsajili kiungo huyo, lilianza kufanywa
kimya kimya ambapo wiki iliyopita Ijumaa viongozi wa Simba walimkalisha
chini na kuzungumza naye ambapo wao walitaka kumpa dolla 20,000 ambazo
Kazimoto alizikataa na kutaka apewe dola 25,000 ambazo Simba wamempa.
Kazimoto yupo nchini kwa muda sasa baada ya timu
yake ya Al Markhiya ya Qatar kuachana naye kutokana na mabadiliko ya
sheria za usajili nchini humo ambazo zinazitaka kila klabu kuwa na
wachezaji watatu wa kigeni.
“Mwinyi amekubali kusaini baada ya viongozi
kukubali kumpa fedha hiyo ingawa wenyewe walikuwa wanataka ashuke
zaidi,” alisema kiongozi huyo.
Usajili wa mchezaji huyo umethibitishwa na Rais wa
Simba, Evans Aveva “Ni kweli amesaini mkataba na tutakuwa naye kwa
kipindi hiki, hiyo imekuja baada ya kufikia makubaliano.”
0 comments:
Post a Comment