Tuesday, June 10, 2014


KOCHA wa Mbeya City, Juma Mwambusi ameona wachezaji kadhaa wa kigeni kwenye michuano ya Mto Nile lakini haruhusiwi kuwasajili kutokana na sera za klabu hiyo.
Alisema sera na uongozi wa timu yake unataka kuibua vipaji vya vijana wa Tanzania  na siyo kuwapapatikia wachezaji wa nje.
“Niliwaona vijana wengi Sudan wenye vipaji vya hali ya juu na nilitamani wachezee Mbeya City, lakini malengo ya timu ni kutaka kuinua vipaji vya vijana wa kitaifa hususan wa Jiji la Mbeya na siyo wachezaji wa kimataifa,” alisema.
Alisema akiwa Sudan aliishia kumezea mate wachezaji wazuri. ‘’Tunasubiri Juni 15 mwaka huu ambapo  tutatangaza usajili mpya wa kikosi chetu, hivyo mashabiki na wapenzi wa Mbeya City wawe na imani na kikosi kitakachotangazwa  kwa msimu ujao.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe