Tuesday, June 10, 2014

Mwenyekiti wa Simba,Ismail Aden Rage.

SIMBA inanunua wachezaji wawili tu wapya wa kigeni, lakini bajeti yake ya usajili mzima wa kikosi ni Sh300 milioni.
Fungu hilo limetengwa na kundi maarufu la Friends of Simba ambalo Mwanaspoti linajua kwamba wanamsapoti Evans Aveva kwenye nafasi ya urais katika uchaguzi ujao wa Juni 29.
Habari kutoka ndani ya klabu hiyo zinasema kwamba kundi hilo limefanya kikao na watu wa Kamati ya Usajili na kutenga bajeti hiyo ingawa baadhi wanadhani inaweza kupungua kufikia Sh250milioni.
Mmoja wa mabosi wa timu hiyo, alisema kiasi hicho cha fedha kitakuwa maalumu kwa ajili ya malipo ya wachezaji watakaosajiliwa sasa na wale wanaoidai klabu hiyo baada ya kubainika kuwa benchi la ufundi limependekeza baadhi ya mikataba ya wachezaji isitishwe.
“Tunaamini kiasi hicho kitatosha kabisa bila matatizo kututafutia wachezaji halisi ambao watarudisha heshima ya Simba, unajua watu wana uchungu na Simba yao,” alisema bosi huyo. “Endapo Michael Wambura atarudishwa katika mbio za uchaguzi, basi ni wazi suala la kusajili litachelewa zaidi mpaka hapo uchaguzi utakapomalizika, lakini wakimwondoa nakuhakikishia baada ya wiki moja tutaanza kusajili rasm

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe