Thursday, June 26, 2014

Man United yaweka mezani mamilioni kumnasa Robben


Supastaa wa Bayern Munich, Arjen Robben.

MANCHESTER United imeripotiwa kuweka mezani kiasi cha Pauni 40 milioni ili kumnasa supastaa wa Bayern Munich, Arjen Robben.
Taarifa ya kutoka kwa mtu wa karibu wa kocha Louis Van Gaal alisema kwamba anaamini winga huyo mwenye umri wa miaka 30 atakuwa mchezaji muhimu sana kwake wakati atakapoanza kibarua chake Man United msimu ujao.
Robben kwa mara ya kwanza alinunuliwa na Van Gaal alipokuwa akiinoa Bayern Munich na baada ya kufanya kazi pamoja kwenye kikosi cha Uholanzi kwenye Fainali za Kombe la Dunia, Mdachi huyo anaamini kwa kiasi hicho cha pesa kilichowekwa mezani kitawashawishi Bayern na kukubali kufanya biashara.
Mwezi uliopita, Robben alikaririwa akiondoa uwezekano wa yeye kuhamia Man United huku akimalizia kwa kusema kwamba kama Bayern watakubali kumuuza basi hawezi kupinga jambo hilo.
Robben alisema amekuwa na furaha Bayern, lakini maisha ya soka yamekuwa yakibadilika kila kukicha kitu ambacho kinaweza kutokea na hivyo msimu ujao akawa ndani ya jezi za Man United.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe