HATARI: Kombe la Dunia 2014 litaondoka na mastaa hawa
Umri wa sasa wa mchezaji huyo ni miaka 36, hadi kufikia fainali zijazo
za Kombe la Dunia nchini Urusi, Drogba atakuwa na umri wa miaka 40 kitu
ambacho kitakuwa kigumu kwake kucheza fainali hizo.
RIO DE JANEIRO, BRAZIL
KIUNGO Mhispaniola, Xabi Alonso, ameripotiwa
kutangaza kustaafu soka la kimataifa baada ya nchi yake ya Hispania
kutolewa kwenye hatua ya makundi katika fainali za Kombe la Dunia
zinazoendelea kule Brazil.
Staa huyo wa Real Madrid amekuwa kwenye kikosi cha
kwanza cha Hispania tangu mwaka 2003 na kufanikiwa kufunga mabao 16
katika mechi 113 alizochezea nchi hiyo na pia kuwamo kwenye vikosi
vilivyotwaa ubingwa wa Ulaya mara mbili mwaka 2008 na 2012 na Kombe la
Dunia mwaka 2010.
Hata hivyo, Alonso ni mmoja tu wa mastaa kadhaa
ambao baada ya fainali hizi za Kombe la Dunia hawataonekana tena kwenye
nchi zao wakati wa fainali zijazo za mwaka 2018 zitakazofanyika Urusi.
Andrea Pirlo, Italia
Kiungo huyo fundi raia wa Italia alitangaza mapema
kwamba atang’atuka kwenye soka la kimataifa baada ya kumalizika kwa
fainali hizi za Kombe la Dunia.
Hata hivyo, kulingana na umri wake wa miaka 35,
Pirlo asingeweza kuwa na nguvu tena ya kucheza fainali zijazo
zitakazofanyika miaka minne baadaye hasa kutokana na soka la kisasa
ambalo limekuwa likichezwa kwa kasi.
Pirlo ambaye pia ni kiungo wa Juventus, amekuwa
kwenye kikosi cha Italia tangu mwaka 2002 na kuwamo kwenye kikosi hicho
kilichonyakua ubingwa wa Kombe la Dunia mwaka 2006. Kwa kipindi chote
alichokuwa na Italia, Pirlo amecheza mechi 111 na kufunga mabao 13.
Didier Drogba, Ivory Coast
Straika Didier Drogba amekwenda kwenye fainali za
Kombe la Dunia nchini Brazil akiwa mmoja wa wachezaji wenye umri mkubwa
katika kikosi cha Ivory Coast.
Umri wa sasa wa mchezaji huyo ni miaka 36, hadi
kufikia fainali zijazo za Kombe la Dunia nchini Urusi, Drogba atakuwa na
umri wa miaka 40 kitu ambacho kitakuwa kigumu kwake kucheza fainali
hizo.
Kwa hali ilivyo, fainali hizi zinatajwa kuwa za
mwisho kwa Drogba na kizazi kingine cha dhahabu cha Ivory Coast ambacho
kimeshindwa kufanya maajabu kwenye michuano ya kimataifa.
RSS Feed
Twitter
11:07 AM
Unknown
Posted in
0 comments:
Post a Comment