
Ripoti zinadai kwamba wacheza kamari wa nchi za
Scandinavia walilifurahia tukio hilo kwa madai kwamba walichokibashiri
kimeibuka kuwa kweli.
Kampuni ya kamari kwa njia ya mtandao ya Betsafe,
walitangaza kwa wacheza kamari kwamba Suarez ambaye alifungiwa kwa
kung’ata wachezaji mara mbili atafanya hivyo tena kwenye fainali za
Kombe la Dunia nchini Brazil.
Inadaiwa kwamba zaidi ya wachezaji kamari 100
walisimamia katika hoja hiyo na ilipotokea kwa Suarez kumng’ata
Chiellini begani kwao ilikuwa wakati wa kulifurahia tukio hilo.
Mshindi mmoja, Jonathan Braeck kutoka
Stenungssund, Sweden, katika dau lake aliweka Dola 12.4 akisema kwamba
Suarez atang’ata mchezaji mwenzake na Braeck sasa anasubiri malipo
mazuri.
“Awali nilikuwa na fikra za kuweka fedha nyingi
lakini rafiki yangu mmoja aliniambia kwamba ninapoteza fedha zangu,’’
alisema Braeck katika mazungumzo na Gazeti la SportExpressen.
“Italia ilipotawala mchezo katika hali ya kawaida
unajua kwamba atakuwa na uchizi fulani, sikufikiria angeng’ata mtu
lakini angefanya jambo la kipumbavu kilichotokea ni kwamba alifanya
jambo la kipumbavu zaidi,’’ alisema.
Betsafe walithibitisha ushindi wa Braeck kupitia
Meneja Masoko wao, Patrik Oqvist kwa kusema: “Tunaweza kuthibitisha
kwamba mteja wetu ameshinda fedha za Sweden Korona 14,000 kwa sababu kwa
mara nyingine, Suarez alimng’ata mchezaji wa timu pinzani.’’
“Tuliliweka hili katika hali ya mzaha lakini inafurahisha kwamba mmoja wa wateja wetu amekuwa sahihi,’’ alisema Oqvist.
Braeck alisema kwamba anatarajia kutumia fedha
alizopata kwenda England kushuhudia mechi za Ligi Kuu lakini hatokwenda
Liverpool kuonana na mtu aliyesaidia kufanikisha safari yake.
“Itakuwa ni safari ya Manchester. Najaribu kutafuta mtu ambaye nitakwenda naye Mancheter United,” alisema.
“Kama nitaipata anuani ya nyumbani kwa Suarez
nitamtumia kadi ya shukurani, ilikuwa jambo zuri kwake kumng’ata mtu na
kunipa safari ya Manchester.”
0 comments:
Post a Comment