Monday, May 5, 2014

UTAJIRI: Fedha za usajili wa Domayo zinaweza kukupa mali hizi

 

KWA mashabiki wa Yanga haikuwa taarifa nzuri. Iliwashitua mno pale waliposikia kuwa kiungo wao mashuhuri, Frank Domayo, amejiunga na mabingwa wapya wa Ligi Kuu Bara, Azam FC kwa mkataba wa miaka miwili.
Domayo alisaini Azam akiwa mchezaji huru baada ya mkataba wake na wana Jangwani hao kubakiza mwezi mmoja tu hivyo kikanuni alikuwa huru kuzungumza na hata kukubaliana na timu nyingine. Kanuni zinatoa uhuru huo kwa mchezaji ambaye amebakiza chini ya miezi sita katika mkataba.
Kiungo huyo anayeichezea pia timu ya taifa, Taifa Stars, ameng’olewa Yanga kwa kitita cha Sh70 milioni huku na pia atakuwa akilipwa mshahara wa Sh3 milioni kwa mwezi achilia mbali posho na juisi za Bakhresa pale Chamazi.
Kwa maisha ya sasa ya Kitanzania, Sh70 milioni alizolipwa ni fedha nyingi na ni wananchi wachache wa nchi hii wanaofanikiwa hata kuzitia tu machoni fedha hizo kabla ya kurudisha roho zao kwa Muumba achilia mbali kuzimiliki.
Hivi ni baadhi tu ya vitu ambavyo unaweza kuvifanya kwa fedha za usajili wa Domayo.
1.Kununua kiwanja
Kiasi cha Sh10 milioni kutoka kwenye kitita hicho kinaweza kukupatia kiwanja cha maana cha ukubwa kati ya mita 25 kwa 25 au hata cha mita 35 kwa 35 katika maeneo tulivu ya Jiji la Dar es Salaam kama vile Tabata, Tegeta, Kimara, Goba au Mbagala.
2.Shamba la ekari 2 Mlandizi, Pwani
Ardhi ni amana kubwa kwenye ulimwengu wa sasa, ni amana ya kudumu. Hivyo ni vyema kwa mtu yeyote kuwekeza kwenye sekta hii kwa ajili ya matumizi yake na ya uzao wake wa baadaye.
Katika fedha za Domayo kwenda Azam, unaweza kutenga kiasi cha Sh 5 milioni pekee kununua kati ya ekari moja hadi mbili za shamba katika maeneo ya Mlandizi au Kigamboni.
3.Toyota Hiace
Wafanyabiashara watakwambia kuwa fedha iliyokaa si sawa na fedha iliyoko kwenye mzunguko. Kwenye fedha za usajili wa Domayo unaweza pia kuchukua milioni 16 na kununua gari aina ya Toyota Hiace kwa ajili ya biashara. Gari hizi zina uwezo wa kuingiza kati ya Sh40,000 hadi 60,000 kwa siku hivyo kuwa kati ya uwekezaji wa maana zaidi kwenye ulimwengu wa sasa unaohitaji zaidi usafiri.

 

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe