Monday, May 5, 2014

Straika mpya Simba msosi sahani tatu na chapati 10

 

Saad Kipanga.

SIMBA iko kwenye harakati kubwa za kumnasa straika wa Mbeya City, Saad Kipanga. Mchezaji huyo anaendelea na mazungumzo ya karibu sana na bosi wa usajili wa Simba, Zakaria Hanspoppe na dili inaweza kufanyika muda wowote  kwani wameshaafikiana vitu vingi.
Yeye amewaambia wampe sh 30mil halafu wamalizane na Mbeya City ambayo ana mkataba nao wa miezi sita. Hayo ni chamtoto sikia sasa mambo ya huyu jamaa.
 Ili ashibe ni lazima apige sahani tatu za chakula zinazojitosheleza, wakati chai yake lazima iwe na chapati 10. Kipanga anayeichezea timu ya Taifa ya Vijana U-20 ‘Ngorongoro Heroes’ ni mdogo kwa umri kwani ana miaka 19, lakini mambo yake hayo ni sawasawa na umbile lake la urefu na kubwa.
Kutokana na sifa hiyo, unaweza kusema Kipanga ametoka ngoma droo na straika wa Simba, Betram Mwombeki ambaye pia ana umbo kubwa na awali aliwahi kusema, ili ashibe ni lazima apige pleti tatu za maana kama Kipanga.
Kipanga mwenye sifa ya kuwa na nguvu za miguu, aliliambia Mwanaspoti: “Siwezi kuficha ukweli wangu, huwa nakula sahani tatu za chakula tena ziwe zimejitosheleza ninapokula, ndiyo nakuwa fiti na kushiba kabisa, tofauti ya hapo, tunakwenda tu.”
“Chai ya asubuhi mara nyingi watu huwa wanakula chapati mbili, hizo kwangu zinapunguza njaa tu, 10 ndiyo mpango mzima, nikila hizo ndiyo nakuwa vizuri,”alisisitiza Kipanga.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe