STEVE NYERERE ATEULIWA KUONGOZA KIKOSI CHA WASANII KUTANGAZA AMANI NCHI NZIMA!
Mwigizaji
na Mchekeshaji ambaye ni Mwenyekiti wa Kundi la Bongo Movie Unity,
Steven Mengere 'Steve Nyerere' (kushoto) akizungumza na waandishi wa
habari (hawapo pichani) jijini Dar es Salaam juzi baada ya kuteuliwa
kuwa msimamizi wa mkuu Wasanii wa nje ya Bunge Maalum, kulia ni Makamu
Mwenyekiti wa Tanzania Kwanza nje ya bunge, Renatus Muadhi, na katikati
ni Mwenyekiti wa Taasisis hiyo, Agustino Matefu.
Mwigizaji
na Mchekeshaji ambaye ni Mwenyekiti wa Kundi la Bongo Movie Unity,
Steven Mengere 'Steve Nyerere' (kushoto) akikabidhiwa mkataba wa kuwa
msimamizi wa mkuu wa wasanii wa nje ya Bunge Maalum na Mwenyekiti wa
Taasisi ya Tanzania Kwanza nje ya bunge, Agustino Matefu. Makabidhiano
hayo yalifanyika juzi jijini Dar es Salaam.
---
---
Na Mwandishi Wetu, Dar es Salaam
WASANII wa Bongo Movie, muziki wa dansi, taarab, maigizo na tamthilia wametangaza kuzunguka nchi nzima wakiwa na kamati ya Tanzania Kwanza Nje ya Bunge Maalum la Katiba kwa lengo la kutangaza amani kwa vijana wa rika lote bara na visiwani.
WASANII wa Bongo Movie, muziki wa dansi, taarab, maigizo na tamthilia wametangaza kuzunguka nchi nzima wakiwa na kamati ya Tanzania Kwanza Nje ya Bunge Maalum la Katiba kwa lengo la kutangaza amani kwa vijana wa rika lote bara na visiwani.
Baadhi ya wasanaii hao ni pamoja na Steven Mengele ‘Steve Nyerere’
ambaye ameteuliwa kuwa msimamizi mkuu wa uwakilishi kwa upande wa
wasanii katika Tanzania kwanza nje ya Bunge maalum, Muungano huo uko
chini ya Mwenyekiti Augustino Matefu.
Akizungumza juzi na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam, Steve
amesema kwamba ataungana na wasanii ambao wako katika vyama mbalimbali
kama vile Chama Cha Demokrasia na Maendeleo, NCCR, Mageuzi , Cuf na
vyama vingine huku wote wakiwa na lengo moja tu la kuhimiza mchakato wa
katiba uendelee huku wanasiasa wakizingatia kudumisha amnai na umoja wa
Watanzania.
Nyerere aliongeza kwa kusema kuwa yeye hakuwa na kipingamizi pindi alipoambiwa amechaguliwa kuwa miongoni mwa wasimamizi wa mpango huo ambao umewakutanisha vijana kutoka katika itikadi mbalimbali za vyama vya siasa.
“Nilipoambiwa hili jambo niliweka itikadi zangu za chama pembeni na kuuvaa Utanzania kwanza ili kuunganisha fani zetu wote kwa pamoja na kuweza kuwahimiza wananchi wadumishe amani tuliyokuwa nayo nchini” alisema Nyerere.
Aliongeza pia kwa kuwaomba viongozi wa dini masheikh na maaskofu wakiwemo mapadri wote kuungana nao wasanii hao katika kuhimizaani ya amani ya nchi.
“Sisi wasanii tunapata riziki zetu kutokana na amani na utulivu uliopo nchini mwetu hivyo kila msanii na Mmtanzania aone ni jambo la fedheha kuiichezea amani ambapo siku ikipitea tutakwenda kuomba hifadhi katika nchi za jirani zilizopata uhuru na kufuata ushauri kutoka kwetu”.,
Aliongeza kwa kusema kwamba ana imani kubwa watanzania watawaelewa pindi watakapokuwa katika ziara hiyo kuzunguka nchi nzima huku wakiwa na mabalozi watano kutoka kila nyanja ya sanaa ambazo ni muziki wa taarab, Hip Hop, Sanaa za maigizo, Michezo na tamthilia. Mkutano mkubwa unatarajiwa kufanyika Kibanda Maiti Zanzibar.
0 comments:
Post a Comment