Sunday, May 11, 2014

Domayo awaponza wachezaji Stars

 

UKIFIKA katika kambi ya Timu ya Taifa ‘Taifa Stars’ mjini Tukuyu unatakiwa ujipange, kwani ulinzi umeimarishwa na wachezaji hawazungumzi ovyo na mtu wasiyemfahamu wakiogopa kuadhibiwa na TFF.
Hali hiyo imekuja baada ya hivi karibuni Frank Domayo kusaini mkataba wa kuichezea Azam akiwa katika kambi hiyo baada ya watu kuingia kinyemela na kumalizana naye.
TFF haikupendezwa na kitendo hicho kiasi cha Rais wake, Jamal Malinzi kuteua mwanasheria wa kuchunguza sakata zima la Domayo.
Mwandishi wa Mwanaspoti, alifika kambini hapo na kukumbana na maswali kadhaa tofauti na awali na hata alipoomba ruhusa ya kuzungumza na baadhi ya wachezaji kutoka kwa Meneja wa Taifa Stars inayojiandaa na mechi dhidi ya Zimbabwe, Clemence Boniface.
‘’Huyu ni mwandishi, anaomba kuzungumza nanyi kuhusu maandalizi yenu, mpeni ushirikiano,’’ alisema Clemence lakini baadhi ya wachezaji walijibu: ‘’Sawa meneja una hakika huyu si wale wanaoweza kutuponza? Maana wengine wanatuponza.’’
Baadhi ya walinzi na wahudumu wa kambi hiyo, walisema tangu sakata la Domayo wachezaji wamebadilika, hawataki kuzungumza na watu  wasiowajua wakihofu kutokea mambo kama hayo

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe