Friday, May 2, 2014

Rooney ajaa wasiwasi Manchester United

STRAIKA, Wayne Rooney amebainisha wasiwasi wake juu ya mpango wa Manchester United wa kutaka kumpa kazi ya ukocha Louis van Gaal kwa sababu jambo hilo litamweka kwenye wakati mgumu na Robin van Persie atapata upendeleo.
Staa huyo wa Man United anaamini Van Gaal na Van Persie ni marafiki wakubwa, hivyo akitua klabuni hapo anaweza kubadili mambo ya kumpanga staa huyo kama chaguo la kwanza kwenye safu ya washambuliaji na hali itarudi kama ilivyokuwa kwa Sir Alex Ferguson msimu uliopita.
Rooney chini ya Ferguson alikuwa chaguo la pili kwenye safu ya ushambuliaji nyuma ya Van Persie jambo lililomfanya staa huyo kutaka kuhama kabla ya David Moyes kuja kumaliza tatizo.
Kwa hali ilivyo kwa sasa, Van Gaal anapewa nafasi kuwa ya kuwa kocha mpya wa timu hiyo jambo ambalo limempa furaha kubwa Van Persie ambaye kwa sasa amerudi mazoezini akitokea kwenye majeruhi katika kipindi cha Moyes.
Van Gaal anaonekana kuwa ndiye kocha mwenye nguvu zaidi ya kutua klabuni hapo baada ya kocha mwingine, Carlo Ancelotti kuwa na uhakika wa kubaki Real Madrid kufuatia kuisaidia kutinga fainali ya Ligi ya Mabingwa Ulaya.

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe