Friday, May 2, 2014

Funga kazi: Hao Man United usipime; Cavani, Strootman na Hummels wakitua ni balaa.

 

KOCHA Mdachi, Louis van Gaal, anapewa nafasi kubwa ya kutua Old Trafford. Familia inayoimiliki klabu ya Manchester United ya Glazer imeweka mezani Pauni 150 milioni kwa ajili ya kufanya usajili tu.
Jambo hilo tayari limeanza kuwatia kiwewe mashabiki wa Man United juu ya mwonekano wa kikosi chao kwa msimu ujao na kuwa na hamu mambo yatakavyokuwa baada ya msimu huu kila kitu kwenda kombo.
Kocha Van Gaal anatarajiwa kutimua mastaa kadhaa klabuni hapo na kuwaleta wengine wapya wachache ambao watakuwa tayari kurudisha makali ya timu hiyo kama zamani.
Hiki ni kikosi cha kufikirika cha Man United itakavyokuwa wakati wa msimu mpya utakaoanza Agosti mwaka huu. Kwa kuanza na wachezaji wapya wanaotarajiwa klabuni hapo na wale wa zamani watakaobaki kikosini.
Edinson Cavani
Straika huyo wa Uruguay kwa sasa anakipiga katika kikosi cha Paris Saint-Germain ya Ufaransa. Thamani yake inatajwa kuwa ni kati ya Pauni 55 milioni hadi 60 milioni.
Cavani hana furaha sana klabuni PSG, hasa kutokana na Zlatan Ibrahimovic ambaye anamfanya apangwe pembeni badala ya nafasi yake anayoipenda ya straika wa kati. Kwa siku za karibuni, Cavani amekuwa kwenye ubora mdogo na hilo lilijionyesha zaidi katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Ulaya dhidi ya Chelsea iliyofanyika Stamford Bridge.
Imeelezwa kwamba watu wa Man United wameshafanya mazungumzo ya awali na wawakilishi wa straika huyo kuhakikisha anang’oka PSG, ambapo klabu hiyo italazimika kuvunja benki yake kwa sababu hatapatikana kwa gharama ndogo.
Cavani alikuwa mchezaji wa sita ghali duniani wakati alipotoka Napoli kwenda PSG kwa uhamisho wa Pauni 52.7 milioni mwaka jana na kama atatua Old Trafford mahali hapo atapata fursa ya kucheza kama straika wa kati kitu anachokikosa PSG.
Luke Shaw
Thamani ya beki huyo kinda wa Southampton inatajwa kuwa Pauni 30 milioni. Kwa muda mrefu Man United imekuwa ikimtaka mchezaji huyo ili kuwa mrithi wa Patrice Evra kwenye beki ya kushoto na wapo tayari kutoa kiasi hicho cha pesa kuipata huduma yake.
Kwa msimu wote, Shaw amekuwa chaguo la kwanza katika kikosi cha Southampton jambo lililozifanya klabu kubwa za Ulaya ikiwamo Chelsea, Manchester City, Bayern Munich na Real Madrid kufukuzia saini yake. Inaaminika kwamba Shaw atakuwa na uhakika wa namba kama atakubali kutua Old Trafford

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe