
Muonekano mpya ya uwanja unaotarajiwa kujengwa na mabingwa wa Ligi Kuu ya England ‘Primiership’ 2013/2014, Manchester City .
Mabingwa wa Ligi Kuu ya England ‘Primiership’ 2013/2014, Manchester
City wanatarajia kujenga Uwanja mpya ambao utakuwa na uwezo wa kuchukua
mashabiki zaidi ya 60,000.
Uwanja wanaoutumia hivi sasa wa Etihad una uwezo wa kuingiza watazamaji 47,620.
Iwapo uwanja huo utakamilika, inamaana kuwa jiji la Manchester
litakuwa na viwanja viwili vikubwa pamoja na kile kinachomilikiwa na Man
United, Old Trafford ambacho kinauwezo wa kuchukua mashabiki 75,000.
0 comments:
Post a Comment