Friday, May 2, 2014

Aliyemrushia ndizi Alves adakwa na polisi

SHABIKI wa Villarreal anayedaiwa kumrushia ndizi beki wa Barcelona, Dani Alves uwanjani Jumapili iliyopita, amekamatwa na polisi nchini Hispania.
Shabiki huyo aliwekwa chini ya ulinzi na kubanwa kwa maswali mazito huku klabu ya Villarreal ikimfungia maisha yake yote kwenda kutazama mechi za klabu hiyo.
Kwenye mchezo huo uliomalizika kwa Barcelona kushinda 3-2 uwanjani Estadio El Madrigal, shabiki huyo alirusha ndizi uwanjani katika dakika ya 75 akimlenga Alves aliyekwenda kupiga kona. Katika kujibu ubaguzi huo, Alves aliiokota ndizi hiyo akaimenya na akaila kabla ya kupiga kona.
Msemaji wa polisi alisema mtu huyo alikamwa na polisi na kuwekwa rumande tangu wikiendi iliyopita.

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe