Monday, April 28, 2014

Van Persie abadili mawazo Man united

STRAIKA, Robin van Persie, amefichua kwamba sasa amefuta mpango wake wa kutaka kuhama Manchester United baada ya klabu hiyo kumtimua David Moyes huku Mdachi mwenzake, Louis van Gaal akitarajia kuwa kocha mpya klabuni hapo.
Ripoti zinabainisha kwamba Van Gaal amekubali kuwa kocha wa Man United baada ya kukutana na mabosi wa klabu hiyo zaidi ya saa 48 zilizopita na kwamba anajiandaa kuwa mrithi wa Moyes klabuni hapo Old Trafford.
Si kitu cha siri kwamba Van Persie amekuwa na urafiki mkubwa na Van Gaal ambaye ni kocha wa timu ya taifa ya Uholanzi na hilo ndilo linalomfanya straika huyo kubadili mawazo yake na kusema ataendelea kubaki Old Trafford msimu ujao.
Van Persie aliweka wazi wiki chache zilizopita kwamba kama Moyes angeendelea kuwa kocha wa timu hiyo, basi angelazimika kutafuta timu ya kuchezea mwisho wa msimu na si kubaki Man United chini ya kocha huyo Mskochi.
Van Persie na Van Gaal wanasimamiwa na wakala mmoja, Kees Vos, ambaye siku chache zilizopita alikuwa kwenye pilikapilika nyingi za mazungumzo na mabosi wa Man United

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe