Ryan Giggs awarudisha pamoja Man United
JUZI Jumamosi, makocha wawili walioingia uwanjani Old Trafford
kupambana kila mmoja akiwa na yake kichwani. Neil Adams wa Norwich City
alikuwa anawaza jinsi ya kukwepa kushuka daraja, Ryan Giggs alikuwa na
presha ya mwanzo wake utakuwaje klabuni Manchester United baada ya
kutajwa kuwa kocha wa muda.
Hata hivyo, hadi kufika mwisho wa dakika 90, mechi
ilikuwa ya upande mmoja na kocha mpya alianza vyema kibarua chake Old
Trafford.
Pengine ameweza kuiongoza Man United kwa mechi
moja tu dhidi ya Norwich, lakini Giggs alitimiza ahadi ya kurudisha upya
makali ya Man United ambayo msimu huu wamefungwa na Stoke City, West
Brom, Swansea, Everton na Sunderland baada ya kushinda 4-0 na kumfanya
mpinzani wake Neil Adams akiwa kwenye hofu kubwa ya kushuka daraja.
Wakati Giggs akiwa anapita kwenye korido za Old
Trafford kuelekea uwanjani kabla ya mechi kuanza, zaidi ya mashabiki
70,000 walilipuka shangwe kumshangilia shujaa wao wakimsapoti baada ya
kupewa kibarua cha kuinoa timu yao. Old Trafford iliungana tena.
Kwenye rekodi yake ya kucheza mechi 962
alizochezea Man United, Giggs amekuwa mchezaji mwenye hadhi kubwa sana
kwenye klabu hiyo kwa karibu miongo miwili yenye mafanikio na
anaendeleza mafanikio. Kwenye mechi yake ya kwanza kama kocha, hata kama
ni kwa muda tu zimekuja kwenye nyakati ambayo Man United ipo pabaya
Ligi Kuu England.
Giggs, 40, Jumanne iliyopita alichaguliwa kuwa
kocha wa muda baada ya David Moyes kutimuliwa, ikiwa ni miezi 10 tu
tangu alipomrithi Sir Alex Ferguson. Kwenye mchezo huo, mashabiki
walidiriki hata kubeba mabango ya kumsifu Giggs na wakidai ndiye hasa
chaguo spesho na si Moyes.
Giggs ni chaguo la wengi katika kuongoza Man
United hadi mwisho wa msimu. Katika kuonyesha miezi 10 ya Moyes klabuni
imashasahaulika, bango lake la ‘The Chosen One’ lililokuwa limewekwa
kwenye jukwaa la Stretford End uwanjani Old Trafford tangu Agosti mwaka
jana liliondolewa mapema sana saa chache tu baada ya kufutwa kazi. Giggs
amerudisha sherehe tena Old Trafford. Man United imeungana tena.
Giggs alipokuwa anaelekea kwenye kiti chake
alionekana kuwa ni kocha wa haja. Alivaa suti na tai yake vizur na
alikuwa akishangiliwa muda wote na mashabiki wa Man United. Alipata muda
pia wa kusaini vitabu vya mashabiki hao.
Ilikuwa rahisi kuona Man United waliamua kuwa
pamoja kumsapoti shujaa wao aliyekuwa nao pamoja kwa miaka yote
waliyotwaa mataji 13 ya Ligi Kuu England kwenye mazingira kama hayo ya
burudani kubwa. Lakini, kwa msimu huu mambo yametibuka, klabu hiyo
itamaliza ligi ikiwa na pointi chache zaidi kwenye historia yao kwenye
ligi hiyo. Hakuna mataji msimu huu na watakosa michuano ya Ulaya msimu
ujao.
Kudhihirisha kwamba wameungana tena kwa pamoja
bila ya kujali hatatwaa ubingwa msimu huu na msimu ujao watakosa Ligi ya
Mabingwa Ulaya, mashabiki walipeperusha bendera uwanjani Old Trafford
na nyimbo za ushindi ziliimbwa kuonyesha umoja umerudi ‘Theatre of
Dreams’ na kuamini kwamba sasa wanaelekea kwenye kuupa kisogo wakati
mgumu klabuni hapo.
Kabla haya ya mechi hali ilionekana kubadilika
klabuni hapo. Giggs aliahidi kurudisha tabasamu kwenye vyuso za
mashabiki na timu ilicheza kwenye ‘mfumo wa United’ na kwa hilo Giggs
alitimiza ahadi yake kwa haraka sana.
Kundi la mashabiki walisikika wakiimba nyimbo za
“United imerudi” hasa baada ya kuonekana kucheza kwa moyo kama
ilivyokuwa enzi za Sir Alex Ferguson. Kwa kuanzia si kitu kibaya na
Giggs alionyesha ishara nzuri na kuwaunganisha pamoja Man United ambao
walionekana kusambaratika kwenye kipindi cha Moyes
RSS Feed
Twitter
10:25 PM
Unknown
0 comments:
Post a Comment