SAID NDEMLA: Yanga watakaa chini Jumamosi
MSIMU huu wa Ligi Kuu Tanzania Bara utamalizika keshokutwa
Jumamosi ambapo timu zote 14 zitacheza mechi zao za kukunja jamvi huku
tayari Azam FC ikiwa imeshatwaa ubingwa.
Azam iliyotinga ligi hiyo kwa mara ya kwanza miaka
saba iliyopita, kwa misimu kadhaa nyuma ilihaha kusaka taji hilo na
msimu uliopita iliishia kushika nafasi ya pili, lakini safari hii
imefanya kweli ikiizidi akili Yanga ambayo ndiyo mshindi wa pili na
Simba ambayo msimu huu imepotea njia. Iko nafasi ya nne.
Katika funga dimba ya ligi, mechi kubwa
inayosubiriwa na wengi ni ile ya watani wa jadi, Simba na Yanga,
itakayochezwa Uwanja wa Taifa jijini Dar es Salaam. Ni mechi ya kulinda
heshima kwa timu hizo pinzani.
Katika mzunguko wa kwanza, timu hizo zilitoka sare
ya mabao 3-3 kwa Simba kufunga mara tatu kipindi cha pili kujikomboa.
Desemba mwaka jana zilicheza tena katika mechi ya Nani Mtani Jembe na
Simba ikashinda 3-1.
Kwa kawaida mechi ya watani hao huvuta hisia kubwa
kuanzia kwa wachezaji, makocha, wanachama na hata mashabiki. Ndivyo
ilivyo na mechi hii pia.
Said Ndemla ni kiungo wa Simba ambaye ametamba
kuifunga Yanga katika mechi hiyo, lakini akisisitiza zaidi kuwa msimu
ujao Simba itakuwa tishio.
Ndemla alisajiliwa na Simba B kwanza akitokea Red
Coast ya Mburahati baada ya kushiriki Kombe la Kinesi na kuonwa na watu
wa Simba ambayo hufanya mazoezi yake uwanjani hapo, Uwanja wa Kinesi.
“Mechi hii kwa ukweli huwa ni ngumu kutabirika,
msimu huu mambo yetu hayajakuwa mazuri, tunajua wanatudharau lakini
ukweli ni kwamba lazima Yanga wafungwe pamoja na ubora wao,” anatamba
Ndemla.
“Kufanya vibaya kwetu hakumaanishi tutafungwa na
Yanga, ni mechi kubwa na tumejipanga kupoza machungu kupitia watani
wetu. Yanga ni walewale tuliokutana nao mzunguko wa kwanza na kwenye
mechi ya Nani Mtani Jembe, hivyo wajiandae kuchapwa, binafsi hakuna
ninayemuhofia Yanga.”
Changamoto binafsi
“Huu ni msimu wangu wa kwanza kucheza Ligi Kuu,
nimekumbana na changamoto nyingi, ligi ngumu na ina upinzani mkubwa na
niliona ugumu mkubwa wa ligi katika mechi yangu ya kwanza na Yanga,”
anasema.
“Nakumbuka mechi ile tulifungana bao 3-3 ambapo
walianza kwa kutufunga na tukarudisha zote, niliingia uwanjani nikiwa na
wasiwasi mkubwa kucheza na Yanga.
0 comments:
Post a Comment