Friday, April 18, 2014

INSHALLAH: Bado mechi nne tu!

 

Kikosi cha Liverpool. LIVERPOOL, ENGLAND

STEVEN Gerrard aliwakusanya wachezaji wenzake huku machozi yakimtoka baada ya ushindi wa mabao 3-2 wa Liverpool dhidi ya Manchester City wa juzi Jumapili na kuwaambia: “Inshallah tutachukua taji.”
Kwa mujibu wa vipaza sauti, Gerrard aliwaambia wachezaji wenzake wasahau haraka matokeo hayo na kujiandaa kwa ajili ya mechi ijayo dhidi ya Norwich City wikiendi ijayo.
“Sikilizeni, mechi hii imepita. Tunakwenda Norwich. Itakuwa hivihivi. Tuko pamoja. Twendeni,” alisikika Gerrard kwa mujibu wa sauti iliyonaswa na vipaza sauti vya uwanjani Anfield.
Mara baada ya mechi hiyo, nahodha huyo alifanya mahojiano na waandishi wa habari na kufafanua alichosema huku akisisitiza: “Nilikuwa na hisia kali, inabidi tuwe watulivu. Kuna mechi nne zinakuja na mechi hizo zina maana kubwa sana.”
Kuhusu ushindi dhidi ya Manchester City, Gerrard alisema: “Hilo ndio onyo kubwa tulilotoa mpaka sasa. Tulionyesha kuwa tunakwenda mpaka mwisho. Hizi ni dakika 90 ndefu zaidi nilizowahi kucheza katika maisha ya soka. Nilikuwa najiuliza sekunde zinasogea vipi. Kuna wakati nilidhani sekunde zilikuwa zinarudi nyuma.
“Hata hivyo haya ni matokeo makubwa kwetu. Tuna mechi nne zilizobaki ambazo kila moja ni kama fainali. Watu wanasema ile ilikuwa mechi kubwa iliyobaki, nawakatalia, mechi kubwa ni dhidi ya Norwich City. Tunawaacha wengine wasema kwamba kombe liko mikononi mwa nani. Wataalamu watasema, lakini hakuna kilicho chetu mpaka sasa.”

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe