Monday, April 21, 2014

Muungano ulivyowavuruga Wazanzibari

 

Hija Hassan Hija akichangia

Wiki hii Watanzania wameshuhudia matukio mengi bungeni. Moja ya matukio hayo ni vita ya maneno na tofauti za kisiasa kati ya CUF na CCM.
Vita hiyo kuhusu aina ya mfumo wa Muungano imewagawa vilivyo Wazanzibari. Kwa siku mbili mfululizo wamevutana juu ya kilichopendekezwa kwao kati ya serikali tatu, mbili au muungano wa mkataba.
Mmoja wa wajumbe hao akawatuhumu Mawaziri wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar (SMZ), kukana misimamo yao ya awali ya kutaka serikali tatu.
Mjumbe aliyeonekana mwiba kwa mawaziri hao ni Hija Hassan Hija.
Pamoja na mambo mengine akasema kabla hawajapewa uwaziri walikuwa wakidai serikali tatu, sasa wanaufyata na kusimama kwenye serikali mbili.
Hija ambaye ni Mbunge wa Jimbo la Kiwani (CUF), aliwatuhumu baadhi ya Mawaziri wa SMZ kuwa ni “wasaka tonge” na wanafiki akisema mawaziri wa aina hiyo ni hatari kwenye jamii.
“Kuna watu wanalinda masilahi yao… iwapo leo Mawaziri wa Zanzibar (akiwaonyesha kwa vidole ndani ya Bunge) utawanyang’anya uwaziri, watadai serikali tatu,” anasema na kuongeza.
“Wenzangu ni mashahidi… Mawaziri wote wa Zanzibar wamekuwa wakisema hadharani kuwa muundo huu wa Muungano unatuonea, leo wamepatwa na nini?” anajibu kwa kusema ni kwa sababu ya masilahi binafsi.
Anabainisha kwamba mawaziri hao ndiyo waliofanya mabadiliko ya 10 ya Katiba visiwani humo, baada ya kauli ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda iliyosema Zanzibar siyo nchi.
Mjumbe huyo anasema amemweleza Waziri, Profesa Mark Mwandosya kuwa mawaziri hao wa Zanzibar hawatetei muungano bali masilahi yao.
“Zanzibar hatuna ubaguzi wa kabila wala dini tuna mgogoro wa wasaka tonge ambao hawajashiba, mkiwafuata hawa muungano huu utakufa, wana mitumbo mikubwa lakini wana njaa,”anaeleza.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais Mipango na Utawala Bora Zanzibar, Mwinyi Haji Makame baada ya kuruhusiwa kuchangia mjadala bungeni akaituhumu CUF kuwa inataka serikali ya mkataba ili ivunje muungano

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe