Chelsea yatia nazi supu ya Liverpool, yaiangusha kichapo kwao Anfield
Straika wa Chelsea, Demba Ba akipita na mpira katikati ya viungo wa Liverpool, Lucas (kulia) na Steven Gerrard (kushoto) wakati wa mchezo wa Ligi Kuu England uliofanyika Anfield jana Jumapili. Chelsea ilishinda 2-0.
MAMBO si mambo Anfield, Chelsea imetia nazi supu ya Liverpool na
sasa imekuwa si supu tena, bali umekuwa mchuzi. Hiyo ni baada ya jana
Jumapili kuwachapa mabao 2-0 kwenye Ligi Kuu England na kuwatibulia
wenyeji hao kasi yao kuelekea ubingwa wa ligi hiyo.
Bao la straika Msenegal, Demba Ba, kwenye kipindi
cha kwanza na jingine la Mbrazili Willian kwenye dakika za lala salama,
yalitosha kwa Jose Mourinho na kikosi chake cha Chelsea kuilaza
Liverpool kwao na kuwatibulia sherehe zao kuhusu ubingwa ambazo tayari
zilikuwa zimeanza Liverpool.
Kwa matokeo hayo, Liverpool sasa inamtihani na
kushinda mechi zake zote mbili zilizobaki, huku ikiomba dua mbaya kwa
Manchester City ambayo bado ina mchezo mmoja mkononi.
Man City baadaye jana ilitarajia kumenyana ugenini
kwa Crystal Palace. Msimamo ulivyo kwa sasa, Liverpool, Chelsea na Man
City yoyote inaweza kuwa bingwa.
Kosa la kiungo na nahodha wa Liverpool, Steven
Gerrard, liliigharimu timu yake kwenye kipindi cha kwanza alipomruhusu
Ba kufunga, kabla ya kupigwa kwa shambulizi la kushitukiza la pasi za
kugongeana kati ya Fernando Torres na Willian na hivyo Mourinho kuondoka
Anfield na pointi zote tatu.
Kwenye mchezo huo, Mourinho alimzidi mbinu
mpinzani wake, Brendan Rodgers kwa kupaki basi muda wote na kushambulia
kwa kushitukiza.
Mchezo mwingine wa ligi hiyo uliochezwa jana
Jumapili, Sunderland iliichapa Cardiff City mabao 4-0 na hivyo
kuendeleza vyema kampeni yao ya kujinasua kutoka kwenye hatari ya
kushuka daraja.
0 comments:
Post a Comment