Tuesday, April 29, 2014

Boat ya Seagul yagonga jahazi.

Boat ya Seagul inayofanya safari zake kati ya Zanzibar na Dar Es Salaam, imegonga jahazi mchana wa leo ambalo lilikuwa likitokea Zanzibar kuja Dar Es Salaam.
Inasemekana kuwa jahazi hilo lilipunguza sana mwendo kutokana na upepo kubadili muelekeo ghafla. Nikiwa mmoja wa mashuhuda tulishangaa kuona Boat ile ikija kwa kasi huku abiria wa kwenye Jahazi wakipunga kuonyesha ishara kuwa hali si salama lakini Boat ilizidi kwenda na mwendo ule ule kana kwamba hakuna kitu mbele yake. na ndipo kishindo kikatokea na Jahazi lile lilikokotwa umbali wa takribani mita 200.
Hakuna aliye fariki kwani abiria wote waliokuwa kwenye jahazi walijitosa baharini kabla ya ajali kutokea isipokuwa wawili ambao walikokotwa na Jahazi lao lakini walifanikiwa kutoka kabla halijazama.
IMG_0727
Tanga la Jahazi likiwa limenasa mbele ya Boat ya Seagul baada ya kugongwa na kuanza kuzama baharini.
IMG_0727
Boat ya Seagul baada ya kuligonga Jahazi ambalo lilikuwa likitokea Zanzibar mchana wa leo.
IMG_0730
Jahazi lianza kuzama baada ya kutokea mpasuko baada ya kugongwa na Boat ya Seagul iliyokuwa ikielekea Zanzibar.
IMG_0732
Sehemu ya Tanga ikionekana kwa mbali huku chombo kikiendelea kuzama baharini eneo la Ferry.
IMG_0734
Ngalawa zikijaribu kuokoa baadhi ya watu waliokuwa kwenye Jahazi ambalo inasemekana lilikuwa limesheheni makreti ya bia na bidhaa nyingine likitokea Zanzibar.
IMG_0737
Wavuvi wakijaribu kuokoa baadhi ya mali kutoka jahazini huku Boat ya Seagul ikiwa imeondoka kuendelea na safari baada ya kuona Jahazi limezama.
Picha hizi haziko clear sana nilipiga kutumia simu yangu ya mkononi.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe