Friday, April 18, 2014

Bingwa wa kupanga sauti, miaka 53 jukwaani, nyimbo zaidi 200

 

Nguli wa muziki wa dansi nchini, Muhidin Maalim Gurumo 

ULIMWENGU wa muziki umekumbwa na mshtuko, kufuatia kifo cha nguli wa muziki wa dansi nchini, Muhidin Maalim Gurumo ambaye amefariki dunia Jumapili iliyopita katika Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) na kuzikwa kijijini kwake Masaki, mkoani Pwani juzi.
Gurumo amefariki kutokana na maradhi ya mapafu na moyo yaliyokuwa yakimsumbua kwa muda mrefu.
Miaka 53 jukwaani
Nguli huyo ambaye ana heshima ya pekee katika ulimwengu wa muziki nchini, amefariki baada ya utumishi wa miaka 53 mfululizo jukwaani akipumzika siku chache zikiwemo siku za Mwezi Mtukufu wa Ramadhani akiwa ametunga na kushiriki kuimba nyimbo nyingi sana.
Aidha, Gurumo ametunga mitindo mitatu ya muziki wa dansi na miwili bado inatamba hadi sasa, mitindo hiyo ni Sikinde unaotumiwa na Bendi ya Mlimani Park na Msondo Ngoma ambao ulikuwa ukitumika na Bendi ya Nutta Jazz (ambayo ilibadilika kwa majina ya Juwata Jazz, Ottu Jazz na sasa Msondo Ngoma).
Mtindo mwingine ni Ndekule ambao ulikufa baada ya Bendi ya Orchestra Safari Sound (OSS) kupotea katika muziki wa dansi na kama si maradhi Gurumo angeshiriki jubilee ya miaka 50 akiwa na bendi hiyo.
Bingwa wa kupanga sauti
Gurumo ameshiriki kutengeneza ‘arrange’ nyimbo mbalimbali zilizotungwa na wanamuziki wengine kwa kuzisahihisha pale alipohisi zina matatizo katika upigaji wa vyombo. Pia alipanga sauti za waimbaji mbalimbali kutokana na maudhui ya wimbo husika na wengi walimwamini katika hilo.
Mwanamuziki huyo alitangaza kustaafu mwishoni mwa mwaka jana, ikiwa ni miezi mitatu kabla ya bendi yake ya Msondo Ngoma haijatimiza miaka 50 ya kuwepo katika ulimwengu wa muziki nchini, amefariki akiwa taswira na nembo ya muziki wa dansi nchini.
Tuzo ya heshima
Tofauti na wakongwe wenzake ambao wamekuwa wakipumzika na kurudi tena jukwaani kama vile marehemu, Fatuma Binti Baraka ‘Bi. Kidude’ kwa kufanya onyesho moja au mawili kwa mwaka, Gurumo ana historia ya namna yake ambayo pengine haiwezi kufikiwa na yeyote nchini na Afrika Mashariki.
Historia inamweka meza moja na wanamuziki wengine nguri duniani kama vile, Mariam Makeba ambaye Rais wa Kwanza wa Afrika Kusini, Nelson Mandela alimtunuku tuzo ya Mama Afrika na Balozi wa Shirika la Umoja wa Mataifa la Kuhudumia Watoto (Unicef), Yosssour Ndour wa Senegal. Pia,

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe