Moyes abakiza siku chache za kumpisha Jurgen Klopp
Kocha David Moyes
Mbaya zaidi alirithi timu ambayo imetwaa ubingwa
wa Ligi Kuu na pia alikuwa na pesa za kutumia kufanya usajili wa nyota
anayemtaka. Wapi palikwenda kombo?
Kwa msimu wake wa kwanza kushindwa kutetea ubingwa
lisingekuwa jambo baya sana, lakini si kushindwa kuwamo kwenye nne
bora. Man United haijawahi kumaliza msimu ikiwa nje ya tatu bora tangu
1991.
Tazama timu kama Everton na Tottenham Hotspur
inapigana vikumbo na Man United kwenye kugombea nafasi ya sita na saba.
Hii ni aibu kwa timu ambayo ina pesa za kutosha za kufanya usajili wa
wachezaji inaowataka. Ni aibu pia kwa klabu kubwa yenye hadhi kubwa kama
ilivyo Man United.
Jumapili hii, Man United itakwenda Goodison Park
kumenyana na Everton kwenye Ligi Kuu England. Kipigo kwenye mchezo huo
kitazima rasmi ndoto za Man United za walau kumaliza nafasi ya nne ili
kufuzu Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao. Kwa msimu huu, timu yoyote
itakayofanikiwa kutwaa ubingwa, iwe Chelsea, Manchester City au
Liverpool, basi shabiki wa Man United atakuwa na swali gumu sana kwa
Moyes.
Mashabiki wake wa zamani katika klabu ya Everton
walishamtabiria kwamba atafukuzwa kazi Old Trafford. Kwa jinsi ambavyo
msimu huu umekwenda ni ngumu kuamini kama Mskochi huyo ataendelea kubaki
kwenye kibarua hicho msimu ujao.
Jurgen Klopp atajwa kuwa mrithi
Gazeti la Daily Mirror limefichua kwamba mabosi wa
Man United kwa sasa wanamfukuzia kocha Jurgen Klopp na kuamini atakuwa
mwafaka wa kumrithi Moyes kwenye klabu hiyo. Kuna kila dalili za Moyes
kusitishiwa ajira yake mwisho wa msimu.
Gazeti hilo la Mirror liliripoti: “United inaamini
mtindo wa soka la Klopp na mbinu zake za ukocha kitu kinachohitajika
sana kwenye klabu hiyo baada ya Moyes kutibua mambo katika msimu wake wa
kwanza.”
Kwenye mchakato huo, Man United pia inahusishwa na
mpango wa kumchukua Mdachi Louis van Gaal. Lakini, mashabiki wa Man
United wanaonekana kufarijika zaidi na kocha Klopp.
Sawa, ni mapema sana kutamka kwamba uteuzi wa
Moyes lilikuwa kosa kubwa. Lakini, bodi ya klabu ya Man United
inafikiria moja ya majina hayo mawili, Klopp na Van Gaal kumrithi Moyes
huku Klopp akionekana kupata sapoti kubwa ya mashabiki wengi kwenye
mchakato wa kupatiwa kibarua hicho.
Man United itasajili nyota inayemtaka.
0 comments:
Post a Comment