Sunday, March 9, 2014

Yaya Toure asema hawezi kwenda Real Madrid

         Supastaa wa Ivory Coast, Yaya Toure anayekipiga katika timu ya Man City nchini England  

HAPANA. Kamwe siwezi na sijawahi kuwaza. Nienda Real Madrid? Haiwezekani. Amesisitiza supastaa wa Ivory Coast, Yaya Toure kwamba kwenye maisha yake hajawahi kuwaza au kufikiria mpango wa kujiunga na Real Madrid ya Hispania.
Kiungo huyo anayekipiga kwenye kikosi cha Manchester City kwa sasa alisema hawezi kwenda Real Madrid kwa sababu moyo wake na mapenzi yake yapo kwa Barcelona, klabu ambayo aliichezea kabla ya kutua England. Yaya Toure alisema Catalunya ndiko moyo wake ulipo na si Madrid.
“Mimi shabiki wa Barcelona, sitarajii kwenda Real Madrid,” alisema Yaya Toure alipozungumza na radio Rac-1 ya Catalan.
Wakati akijiandaa na mchezo wa marudiano wa hatua ya mtoano kwenye Ligi ya Mabingwa Ulaya, Yaya Toure alisema hatashangilia kama ataifunga Barcelona, kwa sababu ni timu anayoiheshimu baada ya kudumu nao kwa miaka mitatu.
“Siwezi kuwakosea heshima. Watu wao siku zote walikuwa wakinisapoti, hivyo siwezi kufanya kinyume. Ninachoshukuru ni kwamba Barcelona wamenifundisha jinsi ya kushinda,” alisema.

 


0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe