Tuesday, February 4, 2014

Yanga na Simba zaingiza Sh139 milioni

Mabeki wa Rhino Ranges Salum Kamana (kushoto) na Ladislaus Mbogo wakimkaba kwa nguvu beki wa Simba, Haruna Shamte (katikati) katika mechi ya Ligi Kuu Bara iliyochezwa jana Jumapili jijini Dar es Salaam. 
By  MWANDISHI WETU  (email the author)
  • Yanga iliyoibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ashanti United pambano lake liliingiza Sh86,035,000 kutokana na watazamaji 14,261. Mechi ya Simba ambayo ilishinda bao 1-0 dhidi ya Rhino Rangers kutoka Tabora iliingiza Sh53,815,000 kwa watazamaji 9,629.

KIBONGO BONGO NOMA

0
Share

MECHI za Ligi Kuu ya Vodacom zilizohusisha timu za Simba na Yanga na kuchezwa Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam wikiendi zimeingiza jumla ya Sh139,850,000.
 Yanga iliyoibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Ashanti United pambano lake liliingiza Sh86,035,000 kutokana na watazamaji 14,261. Mechi ya Simba ambayo ilishinda bao 1-0 dhidi ya Rhino Rangers kutoka Tabora iliingiza Sh53,815,000 kwa watazamaji 9,629.
Mgawanyo kwa mechi ya Yanga ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) Sh13,123,983.05 gharama za kuchapa tiketi Sh2,910,300 wakati kila klabu ilipata Sh 20,650,211.50.
Uwanja Sh10,500,107.54, gharama za mechi Sh 6,300,064.53, Bodi ya Ligi Sh6,300,064.53, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) Sh3,150,032.26 na Chama cha Mpira wa Miguu Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Sh2,450,025.09.
 Mechi ya Simba mgawo ulikuwa Kodi ya Ongezeko la Thamani (VAT) Sh8,209,067.80, gharama za kuchapa tiketi Sh2,910,300 wakati kila klabu ilipata Sh12,595,211.50. Uwanja Sh6,404,344.83, gharama za mechi Sh 3,842,606.90, Bodi ya Ligi Sh3,842,606.90, Mfuko wa Maendeleo ya Mpira wa Miguu (FDF) Sh1,921,303.45 na Chama cha Mpira wa Miguu, Mkoa wa Dar es Salaam (DRFA) Sh1,494,347.13.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe