Thursday, February 6, 2014

Waafrika vijana watakaong’ara Kombe la Dunia 2014

   

                  Huyu ni miongoni mwa waafrika watakaong'ara kombe la dunia 2014

Katika Fainali za Kombe la Dunia 2014, bara la Afrika litawakilishwa na nchi tano ambazo ni Nigeria, Ghana, Cameroon, Algeria na Ivory Coast.
Nchi hizo zote tano zina wachezaji wengi nyota wanaocheza katika Ligi Kuu za nchi mbalimbali barani Ulaya, ambapo wachezaji hao wapo walio na chini ya miaka 22 na wengine ni zaidi ya miaka 22.
Spoti Mikiki inaangalia baadhi ya nyota wa Afrika wenye umri chini ya miaka 22 watakaokuwapo katika Fainali za Kombe la Dunia 2014 na wanatarajiwa kufanya vyema katika fainali hizo, wafuatao ni wachezaji hao:
Ahmed Musa
Ingawa ana miaka 21, Ahmed Musa tayari ni mchezaji muhimu katika klabu yake ya CKSA Moscow ambayo ameichezea mechi nyingi za Ligi Kuu na kimataifa. Mwanzoni mwa mwaka jana akiwa na kikosi cha timu yake ya taifa ya Nigeria alicheza mechi zote hadi timu hiyo ilipotwaa ubingwa wa Afrika.Pia mwaka jana akiwa na klabu yake ya CKSA Moscow alitwaa ubingwa wa Russia
Kijana huyu anatarajiwa kung’ara katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu kutoka na kasi aliyonayo uwanjani na akili ya mchezo wa soka aliyonayo.
Christian Atsu
Atsu (22) amekuwa akipata wakati mgumu wa kupata namba ya kuanza katika kikosi cha timu ya taifa ya Ghana chenye wachezaji wengi nyota wanaocheza soka katika Ligi Kuu mbalimbali barani Ulaya.
Hata hivyo Atsu amekuwa akikibadilisha kikosi cha Ghana kila anapoingia katika kipindi cha pili akitokea benchi.
Hivyo katika Fainali za Kombe la Dunia mwaka huu anatarajiwa kufanya vizuri akiwa bado ana umri mdogo. Mwaka jana Atsu alisajiliwa na klabu ya Chelsea ya England kwa mkataba wa miaka mitano na baada ya hapo ilimtoa kwa mkopo katika klabu ya Vitesse ya Uholanzi.
Fabrice Olinga
Wakati mshambuliaji wa timu ya taifa ya Cameroon na klabu ya Chelsea, Samuel Eto’o akiwa anaelekea kustaafu kucheza soka, Cameroon hivi sasa inawandaa vijana wadogo wawili ambao wote wanacheza soka katika Ligi Kuu ya Hispania. Wachezaji hao ni Fabrice Olinga na Jean Marie Dongou.

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe