Simba, Yanga staili mpya
Kocha Hans akitoa maelekezo kwa mchezaji wake wa Yanga
KATIKA kuhakikisha wachezaji wao wanashika mafunzo kikamilifu,
makocha Wazungu, Zdravko Logarusic (Simba) na Hans Pluijm (Yanga),
wamekuja na staili za kisasa zaidi ambazo ni ngeni kwa timu za soka za
Tanzania.
Makocha hao wamekuwa wakifundisha kwa staili
mbili, kwanza wanaanza kwa kusisitiza vitendo na baadaye wanatumia ubao
wa kuandikia kuwaelekeza wachezaji kwa karibu zaidi ili kila mmoja
aelewe kiundani.
Staili hiyo imekuwa ikitumiwa na makocha hao tangu
waanze kazi kwenye timu hizo kongwe ambazo zinapashia kwenye viwanja
vya kuazima.
Kwenye Uwanja wa Kinesi, Ubungo jijini Dar es
Salaam, Logarusic amekuwa akitumia ubao kwa dakika kumi kuwafundisha
wachezaji wake baada ya kusimamisha mchezo na kuwakusanya, wachezaji
humzunguka.
Kwa upande mwingine, Pluijm amekuwa akitumia muda
wa dakika 15 katika mazoezi yake kwa ajili ya kuzungumza na wachezaji
kwa karibu zaidi na kutoa maelekezo kwa maandishi ubaoni.
Yanga iliyokuwa ikifanya mazoezi kwenye Uwanja wa
Karume jijini Dar es Salaam inaondoka leo Alhamisi kwenda Comoro
kurudiana na Komorozine katika mechi ya Ligi ya Mabingwa Afrika.
Pluijm amekuwa akiwasimamisha wachezaji sehemu
moja na huku akizungumza nao na wakati mwingine kumwelekeza mmoja mmoja
pembeni akisaidiwa na Kocha Msaidizi, Boniface Mkwasa. Amekuwa
akiwaelekeza makosa ambayo ameyaona ndani ya uwanja na namna ya kufanya
ili wafanikiwe zaidi na wakimaliza, wanafanya mazoezi ya mwisho kwa
vitendo.
Akizungumza na Mwanaspoti, Mkwasa alisema:
“Tunafanya hivi kwa ajili ya kuelekezana upungufu na namna ya kuutatua,
kama tutafanya tu mazoezi ya kucheza bila darasa hatuwezi kufanikiwa.”
0 comments:
Post a Comment