Thursday, August 13, 2015


KOCHA Mwingereza, Dylan Kerr, alipewa mkataba na Simba mwishoni mwa Juni. Baada ya kama wiki hivi akaenda mazoezini pale Chang’ombe. Alipofika kitu cha kwanza kilichomshtukiza ni aina ya uwanja aliokuta wachezaji wanafanyia mazoezi. Lakini baadaye akakausha.
Akatumia kama siku tatu hivi kusoma wachezaji lakini ndani ya huo muda uso wake ukaonyesha anatafakari sana. Akawaambia viongozi timu iende Tanga apate muda wa kuwasoma jamaa vizuri. Viongozi wakamuuliza unaonaje mziki wetu? Akajifanya kama hajasikia akawaambia kaeni hapo niwaambie kitu.
Wakamtajia makipa akawaambia nataka mniongezee mmoja, wakaingia kwenye beki akasema anataka pia mpya mmoja, kiungo akakuna kichwa kidogo akawaambia wamuongezee pia mmoja. Ilipofika kwenye mastraika sasa akawambia acheni masihara inabidi tuingie mfukoni tusajili.
Jamaa mmoja akamwambia hata yule (anamtaja) na ...(anamtaja pia ) ina maana hawafai? Mzungu akamwambia mimi ndiye kocha nataka straika. Baada ya mechi na SC Villa mzungu akamuita chobisi kiongozi mmoja akamwambia umeona nlichokwa namaanisha? Nafasi 14 unafungaje bao moja? Jamaa akasema ni kweli aisee ngoja tukajipange.
Simba ikafanya mishemishe na kuwaleta nchini straika Mrundi Kevin Ndayisenga na Makan Dembele raia wa Mali ambao walianza mazoezi na timu hiyo jana Jumatano.
Dembele aliwahi kutamba na Raja Cassablanca ya Morocco miaka ya nyuma na taarifa kutoka katika mitandao zinaonyesha kuwa mara ya mwisho aliichezea JS Kabylie ya Algeria mwaka 2013. Ndayisega anatokea Atletico ya Burundi.
Kerr ameomba kuwaona mastraika hao wawili katika mazoezi yake kwanza kabla ya kuwapa ruhusa viongozi kukamilisha usajili wao kutokana na kuwepo kwa wasiwasi wa kusajili mastraika wa viwango vya kawaida.
“Nimewaomba viongozi wasifanye usajili kwanza, walete wachezaji tuwaone na hata hao wawili inabidi nijiridhishe na uwezo wao kwanza, tunahitaji mtu makini katika ufungaji,” alisema Kerr ambaye amemkataa Elius Maguli na kuwaambia viongozi wampeleke kwa mkopo popote ingawa baadhi yao bado hawaamini uamuzi huo.
Rais wa Simba, Evans Aveva alikiri kuwa bado wana kazi kubwa ya kukamilisha usajili huo wa straika lakini kocha ndiye mwenye uamuzi wa mwisho baada ya kuwaona wale watakaofanya majaribio.
“Lengo letu kubwa ilikuwa kwa Mavugo lakini dili likakwama, sasa tumemwachia kocha atoe uamuzi juu ya hawa waliopo, ni kweli timu inahitaji straika,” alisema Aveva ambaye ameasisi mauzo ya jezi halali za Simba ambapo moja huuzwa 15,000.
Simba inaumiza kichwa kwa sasa kupata straika makini atakayeweza kuzitumia vizuri nafasi zinazotengenezwa na timu hiyo baada ya mastraika waliopo kushindwa kumvutia vilivyo Kerr.
Awali timu hiyo ilifanya mazungumzo na straika wa Vital’O ya Burundi, Laudit Mavugo ambaye alikubali kutua Msimbazi kabla ya baadaye kuzuiwa na rais wa timu

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe