Thursday, August 7, 2014

ALIYEKUWA mchumba wa msanii wa filamu Bongo, marehemu Sheila Haule ‘Recho’, George Saguda amesema baada ya kumalizika kwa mfungo wa mwezi mtukufu wa Ramadhan, sasa anajiandaa kwa ajili ya kisomo cha kumkumbuka mwenzake huyo.

Marehemu 'Recho' na aliyekuwa mpenzi wake George Saguda wakiwa ni wenye furaha pamoja enzi za uhai wake.
Akipiga stori na gazeti hili, Saguda alisema zilipotimia siku 40, kilifanyika kisomo kwa bibi wa marehemu huko Songea, lakini kwa vile Recho alikuwa akiishi Dar es Salaam na wasanii wenzake wapo huko, yeye anajipanga kufanya kisomo maalum kwa ajili ya mchumba wake huyo ambaye hawezi kumsahau milele.
“Baada ya Ramadhani kumalizika nitafanya kisomo kwa ajili yake na mwanangu ili Mungu awapunguzie adhabu ya kaburi, pia kwa walioenda kuweka tunguri kwenye kaburi lake, kama walikuwa na nia mbaya Mungu aepushe maana nikisema niende kwa waganga nitakuwa napoteza muda tu kikubwa namtegemea Mungu,” alisema Saguda.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe