Wednesday, June 18, 2014


KATIKA kujiongezea vyanzo vya mapato, staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma ameamua kujizatiti zaidi kwenye biashara ambapo sasa amefungua sehemu ya kuoshea magari maarufu kama Car Wash iliyopo Tabata, Dar es Salaam.

Staa wa filamu za Kibongo, Wastara Juma akiosha moja ya gari lililofika kupata huduma ya uoshaji katika 'Car Wash service station' yake iliyopo Tabata, jijini Dar es Salaam.
Akizungumza katika uzinduzi wa car wash hiyo aliyoipa jina la Mamii Car Wash, Wastara alisema ameamua kujiimarisha zaidi kibiashara kwa kuwa soko la filamu kwa sasa lipo chini na lina mikikimikiki mingi.
Huu ni mwonekano wa kituo cha Wastara cha kuoshea magari.
“Hakuna cha maana ninachopata kwenye filamu zaidi ya umaarufu tu. Wakati marehemu mume wangu (Sajuki) alipokuwa hai alikuwa anakimbizana kuhakikisha mambo yanakwenda sawa lakini mimi kama mtoto wa kike, nashindwa kufuatilia vizuri.
“Kwa sasa nimeamua kujikita zaidi kwenye biashara, filamu nitafanya lakini mara chache. Hapa nasubiri Ramadhani ianze na ipite, natarajia kufungua na hoteli hapahapa baada ya mfungo,” alisema Wastara.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe