SHULE YA MWALIMU NYERERE YAVAMIWA NA KUNGUNI
Akizungumza na waandishi wetu, Mwalimu Mkuu Msaidizi wa shule hiyo, Agustino Angelo, alisema tatizo hilo limekuwepo muda mrefu na wamejitahidi kulipunguza kwa kiasi kikubwa kwa kufanya upuliziaji (fummigation) mara mbili huku naye Mstahiki Meya wa Ilala Jerry Slaa, akiahidi kulimaliza kabisa tatizo hilo katika siku za hivi karibuni.
Waandishi wetu walizungumza na baadhi ya wanafunzi wa shule hiyo, ambao walikiri kusumbuliwa na tatizo hilo ambalo wanadai kuwa linawakosesha amani na kuwataka viongozi wa serikali wajitokeze kutokomeza tatizo hilo ili waendelee na masomo yao vizuri.
Mbali na hayo, waandishi wetu pia walishuhudia majengo chakavu ya shule hiyo, mazingira ambayo si rafiki na heshima ya shule hiyo yenye historia kubwa nchini.
0 comments:
Post a Comment