Friday, May 16, 2014


Wema na Kajala wakiwa katika picha ya pamoja kabla ya kuanza kwa bifu yao iliyopelekea waanze kuonana kama paka na panya

KINACHOGOMBEWA baina ya waigizaji wawili wa Bongomuvi, Wema Sepetu na Kajala Masanja, ambao awali walikuwa maswahiba wakubwa hakijajulikana mpaka sasa.
Kila mmoja anamrushia mpira mwenzake kwamba ndiye mwenye makosa na mwanzilishi wa sekeseke ambalo limewagawanya mashabiki pande mbili.
Maneno yameendelea kurushwa na watu wasiofahamika ikidaiwa kuwa wahusika ni wasanii hao. Hivi karibuni Kajala alisafiri kwenda China na safari ikazua maneno lukuki kwamba ilikuwa ikimhusisha pia mpenzi wa zamani wa Wema.
Mpaka sasa mwigizaji huyo inasemekana yupo na mtu huyo licha ya kwamba hakuna ushahidi kuhusu hilo. Vyombo mbalimbali vya habari vimeripoti kuwa vinamsubiri mwigizaji huyo Uwanja wa Ndege wa Mwalimu Nyerere kumhoji kwa kitendo anachodaiwa kumfanyia swahiba wake.
Kwa upande wa Wema, yeye ameendelea kushikilia msimamo wake kwamba hana ugomvi na Kajala licha ya kuonekana akiposti picha wakiwa pamoja kama afanyavyo Kajala. Hali hiyo imeufanya ugomvi wao kuonekana kuwa ni wa chinichini mno.
Wawili hao walianza urafiki wao tangu Wema alipomlipia mwenzake faini ya Sh13 milioni mahakamani na kumwepusha kwenda jela baada ya kuhukumiwa kifungo cha miaka saba.
Kajala alitakiwa kulipa faini hiyo baada ya kupatikana na hatia ya kuuza nyumba iliyokuwa imewekwa rehani kisheria. Nyumba hiyo iliwekwa rehani kutokana na mume wa Kajala, Faraja Agustino, kushtakiwa kwa kosa la kutakatisha fedha haramu.
Chanzo
Taarifa zilianza kwamba wawili hawa wanamgombea aliyekuwa mpenzi wa Wema wa zamani aliyefahamika kwa jina moja la Clement, ilisemekana kwamba Kajala anatoka na huyo mtu japo mpaka sasa hakuna ushahidi wa jambo hilo japo baadhi ya watu wameendelea kusema ni kweli na wameshawaona wawili hao sehemu mbalimbali jijini Dar es Salaam.
Ugomvi huo ulianza wakati Kajala akitengeza filamu yake ya pili inayoitwa ‘Pishu’ aliyomshirikisha Mzee Senga chini ya mtayarishaji Lamata.
Wakati wakimalizia filamu hiyo maeneo ya Block 41 huku Kajala akiwa bibi harusi akimpakia Mzee Vengu kwenye baiskeli, Kajala alilowa sana jasho na kuamua kupitia Saloon maeneo ya Kinondoni Makaburini na ndipo alipokutana na Wema.
Chanzo hicho kilieleza kuwa Wema alitaka kumkumbatia, lakini Kajala alikataa na kumzuia kwa mkono kwa sababu ya jasho na ndio hapo rafiki yake hiyo hakuonyesha kufurahi kwa kitendo kile.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe