Friday, May 2, 2014

Pep Guardiola ajibebesha lawama kichapo cha Bayern

 

Pep Guardiola  

PEP Guardiola amekubali yaishe na kujibebesha lawama zote baada ya Bayern Munich kutupwa nje ya Ligi ya Mabingwa Ulaya kwa aibu kubwa kufuatia kuchapwa na Real Madrid mabao 4-0 uwanjani kwao Allianz Arena juzi Jumanne usiku.
Kwa kipigo hicho kilichowafanya miamba hiyo ya Ujerumani kuutema ubingwa wa Ulaya, timu hiyo imekomea nusu fainali wakiwa wamechapwa mabao 5-0, kitu kinachotazamwa na Wahispaniola kama kisasi baada ya msimu uliopita timu hiyo kuitupa nje Barcelona kwa jumla ya mabao 7-0 katika hatua kama hiyo.
Kwenye mchezo huo, Guardiola na kikosi chake walipata somo kubwa juu ya soka la kushambulia kwa kushtukiza ambalo lilichezwa na Real Madrid chini ya kocha wake, Mtaliano Carlo Ancelotti.
Mastaa Sergio Aguero na Cristiano Ronaldo kila mmoja alifunga mara mbili kuwadhalilisha mabingwa hao wa Ulaya mbele ya mashabiki wao uwanjani Allianz Arena na kocha Guardiola alisema waliadhibiwa kwa sababu walishindwa kuufanyia haki mpira wakati ulipokuwa kwenye miguu yao.
“Sababu kubwa ya kufungwa kwetu ni kwa sababu hatukuwa na mpira sana. Kule Manchester na hata Madrid tulikuwa vizuri sana uwanjani, lakini si kwenye mechi hii,” alisema Guardiola.
“Kama unashindwa kumiliki mpira, basi huwezi kuwa na nafasi unapocheza na timu kama hii (Real Madrid).
“Tulicheza vibaya na hilo ni wajibu wangu. Tulikuwa juu sana na kichapo hiki ni ajabu. Nitakachofanya sasa mazoezini ni kurudisha morali ya wachezaji ndani ya timu.”

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe