Wednesday, May 7, 2014

 

Mr Rage

KWA mujibu wa Katiba mpya ya Simba, Mbunge wa Tabora Mjini, Ismail Aden Rage, sasa ni Rais wa klabu hiyo.
Katiba ya Simba iliyokuwa kwa Msajili wa Klabu na Vyama vya Michezo nchini imepitishwa rasmi huku cheo cha Mwenyekiti ambacho Rage anacho kimebadilishwa na kuwa Rais. Rage ndiye Mwenyekiti kwa sasa.
Kupitishwa kwa Katiba hiyo pia kunamaanisha kuwa zoezi la uchaguzi wa klabu ya Simba limefunguliwa rasmi na leo Jumanne Kamati ya Uchaguzi ya timu hiyo itakutana ili kujadili tarehe rasmi ya kufanyika kwa uchaguzi huo pamoja na utaratibu utakaotumika.
Akitangaza kupokea katiba hiyo mpya Toleo la mwaka 2014, Katibu Mkuu wa Simba, Ezekiel Kamwaga alisema kipengele cha 26 kilipendekezwa na wanachama wa klabu hiyo kumruhusu mtu aliyewahi kushtakiwa kwa makosa ya jinai kugombea, kiliondolewa na kurejeshwa kile cha awali kilichokua kikitaza suala hilo kama ilivyoelekezwa na TFF.
Katibu huyo aliongeza kuwa katiba hiyo mpya pia imeongeza kipengele cha Kamati ya Maadili na Rufaa ambayo itatangazwa wiki hii na itakua ikishughulikia masuala ya maadili pamoja na kutoa fursa ya wanachama wa timu hiyo kukatia rufaa maamuzi mbalimbali ambayo hawajaridhishwa nayo.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe