Sunday, April 6, 2014

Rooney akiri kuumizwa na Liverpool msimu huu

STRAIKA, Wayne Rooney wa Manchester United amesema inamuuma sana na kwamba yupo kwenye wakati mgumu wa kuvumilia mafanikio ya mahasimu wao Liverpool kwenye Ligi Kuu England msimu huu.
Liverpool imekuwa kwenye ubora mkubwa msimu huu na kupata nafasi za juu kwenye msimamo wa ligi hiyo tofauti na Man United ambayo ipo kwenye nafasi ya sita.
Klabu ya Liverpool ipo kwenye nafasi ya pili katika msimamo wa ligi, pointi saba nyuma ya vinara Chelsea, lakini wao wakuwa na mchezo mmoja mkononi.
Lakini, kwa upande wa Man United hadithi imekuwa tofauti baada ya timu hiyo kuwa nyuma kwa pointi tisa kwenye kuifikia nne bora na hivyo kuzidi kujiweka kwenye wakati mgumu wa kushiriki Ligi ya Mabingwa Ulaya msimu ujao.
“Kuwatazama Manchester City wakifanya vizuri, sambamba na Liverpool ni kitu kinachoumiza sana,” alisema Rooney.
“Si kitu kizuri hasa ukijifahamu kwamba unaweza kufanya kitu fulani kwenye ushindani na kisha unashindwa kufanya hivyo. Tunalifahamu hilo na ndio maana dhamira yetu ya msimu huu ni kuhakikisha tunamaliza ligi kwa nguvu sana.”
Man United itamenyana na Liverpool kwenye Ligi Kuu England uwanjani Old Trafford, Jumapili hii

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe