Sunday, April 6, 2014

Aliyeiua Man Utd sasa bondia hatari

LONDON, ENGLAND
MAISHA yanaenda kasi na yanabadilika kwa haraka zaidi. Leon McKenzie, staa wa Norwich City aliyemliza Sir Alex Ferguson katika pambano la Ligi Kuu England mwaka 2005 sasa ni mmoja kati ya mabondia hodari Uingereza.
Jumamosi iliyopita, McKenzie alimtwanga bondia Nikola Varbanov katika raundi ya pili kwenye Ukumbi wa York Hall na kuendeleza rekodi yake ya kutopigwa pambano lolote katika mechi nne alizocheza katika ngumi za kulipwa.
Katika pambano hilo ambalo Man United ilikufa 2-0 katika Uwanja wa Carrow Road, McKenzie alikiliza kikosi cha Sir Alex Ferguson kwa bao murua la pili huku mastaa wa Man United, Cristiano Ronaldo na Wayne Rooney wakishangaa.
“Alikuwa Rooney ndiye aliyepoteza mpira, Youssef Safri aliuiba kutoka kwake na kuupeleka pembeni kwa Darren Huckerby aliyepenyeza mpira kwa Deano na nikamalizia kwa umaridadi,” anasema McKenzie.
“Nakumbuka wakati timu zikiingia nilimpiga jicho kali Rio Ferdinand halafu nikajisemea: “leo nitakuonyesha.” Katika soka unahitaji kwenda uwanjani na kushindana nao. Kuna watu wengine wananywea, lakini mimi nimetoka katika familia ya ngumi kwa hiyo najua kupandisha kiwango katika wakati mwafaka.”
Aingia katika soka baba akiwa bondia
Leon ni mtoto wa bondia bingwa wa zamani wa England na Ulaya, Clinton McKenzie pia baba yake mdogo, Duke McKenzie akiwa bingwa mara tatu wa zamani wa ubingwa wa dunia.
Leon alianza kucheza soka katika klabu yao ya mtaani Crystal Palace na mwishowe kusajiliwa katika timu ya wakubwa kuanzia mwaka 1995 hadi 1996. Mwaka 1997 alitolewa kwa mkopo kwenda Fulham na mwaka 1998  akaenda zake Peterborough United, ambako alifunga mabao tisa katika mechi 15.
Mwaka 2003 alihamia Norwich City ambako alitengeneza jina kubwa kiasi cha kuchaguliwa kuwa mwanasoka bora wa tatu wa klabu katika msimu wa 2004–05, akiwa nyuma ya Darren Huckerby na Damien Francis.
Msimu wa 2005–06 Leon alijikuta katika wakati mgumu kutokana na kukabiliwa na majeruhi huku pia akikumbana na wakati mgumu katika maisha yake binafsi huku akiachana na mkewe.
Mwanzoni mwa msimu wa 2006–07, Leon alimkabidhi barua ya kuomba kuuzwa kocha wa wakati huo wa Norwich, Nigel Worthington lakini kocha huyo alikataa maombi hayo huku akidai kwamba klabu hiyo ingemuuza McKenzie kwa timu ambayo ingetoa ofa nono

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe