Monday, April 28, 2014

Niyonzima abakizwa Yanga kwa masharti

 

kiungo wa timu ya Yanga Haruna Niyonzima  

YANGA inapiga hesabu ni nyota gani wanaotakiwa kuachwa katika msimu ujao, lakini jina la kiungo Haruna Niyonzima limepona baada ya kuingia makubaliano maalumu na benchi la ufundi.
Taarifa kutoka ndani ya benchi hilo na kamati ya usajili, imesema katika ripoti iliyowasilishwa na kocha, Hans PLuijm, imeonyesha kwamba Niyonzima bado anahitajika katika kikosi hicho, lakini akapewa kazi moja ya kuhakikisha analifanyia kazi tatizo la kutokaa na mpira muda mrefu kitu ambacho makocha hao hawakitaki.
Bosi mmoja mzito kwenye kamati ya usajili, alisema Niyonzima ambaye bado ana mkataba wa msimu mmoja na Yanga, ameonyesha kukubalika na benchi lao la ufundi ambapo sasa anatakiwa kuhakikisha anakubaliana na mabadiliko hayo aliyotakiwa kuyafanya.
"Ripoti inaonyesha kwamba Niyonzima bado yupo katika mipango ya kocha na hata mimi nilizungumza na kocha mkuu (Pluijm) alisema hawezi kumuacha mchezaji kama huyo kirahisi, isipokuwa ametakiwa kubadilika katika kukaa sana na mpira ni kitu ambacho makocha hawakitaki," alisema bosi huyo.
Mwanaspoti lilimtafuta Niyonzima ambaye alikiri kuzungumza na Pluijm ambaye amemtaka kulifanyia kazi hilo.
"Nasikia tu katika vyombo vya habari taarifa zangu kuwa naachwa, najikuta nashangaa. Ni kweli kuwa kocha amenitaka kubadilika hakuna njia ya mkato kwamba inabidi nilifanyie kazi, ni mambo mengi tu nimezungumza naye," alisema

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe