Moyes, mkewe wanaswa na mabegi yao Marekani
Moyes akiwa na mabegi akiwa na mkewe
KOCHA, David Moyes, anataka kusahau majanga yake yaliyomkuta
Manchester United baada ya kumchukua mkewe, Pamela na kwenda mapumzikoni
Miami, Marekani.
Baada ya kocha huyo kufutwa kazi Man United
Jumanne iliyopita na kisha Ryan Giggs kukabidhiwa majukumu ya kuinoa
timu hiyo hadi mwisho wa msimu na huku Man United ikiishinda Norwich
City juzi Jumamosi kwenye Uwanja wa Old Trafford, Moyes alionekana
Florida kwenye mgahawa mmoja akipata chakula cha jioni na mkewe.
Mwanzoni Moyes na Pamela walionekana na mabegi yao
jijini Manchester wakiwa hawaeleweki wanakwenda wapi kabla ya picha za
Jumamosi kuwaonyesha wakiwa Miami, Florida akijipumzisha kupoteza mawazo
ya kufukuzwa kazi.
Akiwa kwenye meza ya chakula na mkewe, Moyes, mara
kadhaa alionekana kubofyabofya simu yake huku wanoko wakidai kwamba
alikuwa akitazama matokeo ya timu hiyo kwenye mechi yao dhidi ya Norwich
City. Man United ilishinda 4-0
0 comments:
Post a Comment