Monday, April 28, 2014

Kumbe Van Gaal ni mwendawazimu namna hii!

 

WAKATI Manchester United itakapomtangaza, Lous Van Gaal kuwa kocha wao mpya pale Old Trafford, usije ukadhani kwamba watakuwa wamemchagua kocha mstaarabu na mpole. Hapana, watakuwa wamemchagua kocha mwendawazimu aliyepitiliza.
Awavulia bukta wachezaji wake
Kama maigizo hivi. Lakini katika tukio moja lililotokea wakati wa msimu wa 2009/10 akiwa na Bayern Munich ya Ujerumani, Van Gaal alifanya kituko cha ajabu kwa kuvua suruali yake mbele ya wachezaji wa Bayern kuwaonyesha kuwa yeye alikuwa mwanamume shababi na mwenye makende. Mshambuliaji wa zamani wa Italia, Luca Toni, anaelezea tukio hilo.
“Kocha alitaka kutuonyesha wazi kwamba anaweza kumwacha nje mchezaji yeyote yule. Alitaka kuashiria kwamba alikuwa na kende. Alifanya hivyo kwa kuvua suruali yake. Sikuwahi kuona kitu kama hicho maishani, ulikuwa ni ukichaa. Sikuona vizuri sehemu zake za siri kwa sababu sikuwa mbele,” anasema Toni.
Kwa mtindo huu, Wayne Rooney na Robin Van Persie wajiandae!
Amfukuza Rivaldo Barcelona
Wakati Van Gaal aliporudi Barcelona mwaka 2002, moja kati ya kazi zake za kwanza ilikuwa kumfukuza Rivaldo, mchezaji ambaye hakuwa na uhusiano naye mzuri kabisa. Hii ilikuwa ni moja kati ya majibu yake kwa Rivaldo ambaye aliwahi kukaririwa na vyombo vya habari akisema: “Simpendi Van Gaal na Van Gaal hanipendi.”
Baadaye Van Gaal aliripotiwa akidai kuwa madai ya Rivaldo hayakuwa ya kweli.
“Nampenda Rivaldo hasa yule wa kabla ya kutwaa uanasoka bora wa Dunia mwaka 1999. Nilimpenda Rivaldo. Nilimpenda sana kwa sababu alikuwa bora. Lakini kuanzia hapo kwenda mbele hakuweza kuhimili mapigo. Si katika soka tu, bali hata katika maisha yake binafsi. Hata ukiangalia kwa makocha wengine, kiwango cha Barcelona kimeporomoka,” alisema.
“Nilimpenda Ronaldo aliyejituma. Kwa sasa hajitumi kabisa. Kiwango chake Barcelona kimeshuka tofauti na anapokuwa na Brazil. Nilipomwona Rivaldo na Brazil alikuwa ana njaa, anajituma.”
Aidharau Barcelona
Van Gaal alipata mafanikio makubwa akiwa katika soka la kwao Uholanzi ambako alitwaa Kombe la Uefa, taji la Ligi ya Mabingwa Ulaya na mataji matatu ya Ligi Kuu Uholanzi ‘Eredivisie’.

 

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe