Monday, April 28, 2014

Hekta 9,000 zatengwa kwa kilimo cha mpunga Rufiji

                      

                                           Waziri Christopher ChizaSerikali  imetenga hekta 9,000 kwa ajili ya kilimo cha mpunga Wilaya ya Rufiji mkoani Pwani katika utekelezaji wa mpango wa Uwekezaji mkubwa wa kilimo katika mikoa ya Kusini (Sagcot).

Akizungumza na wakazi wa kata ya Kipugila, Mkurugenzi wa Saggot, Godfrey Kirenga, alisema mradi huo upo katika eneo la Rukililo na utakuwa na uwezo wa kuzalisha tani 250,000 za mpunga kwa mwaka.

Kirenga alisema eneo lilotengwa kwa ajili ya kilimo hicho inajumuisha vijiji vya Ndundunyikanza, Nyaminywili, Kipo na Kipugila.

Alisema idadi hiyo imegawanywa katika sehemu kuu mbili, ambapo hekta 5,000 atapewa mwekezaji mkubwa na hekta 4,000 watamilikishwa wananchi wa vijiji hivyo.

Kirenga alisema kwa sasa Tanzania inazalisha tani milioni 1.2 kwa mwaka, hivyo kiwango hicho kitaifanya nchi kuwa kituo kikuu cha chakula katika Ukanda wa Afrika Mashariki.

"Nia ya serikali ni kutajirisha wananchi kwa kupitia kilimo katika mpango huu wa Sagcot mkulima atakuwa na uhakika wa kupata soko pamoja na uwezeshaji wa kilimo shadidi cha mpunga," alisema.

Aliwataka wananchi wa maeneo hayo kushiriki kikamilifu na kuendelea kuunga mkono mpango huo wenye lengo la kuwakomboa dhidi ya umaskini.

Alisema kilimo kama hicho kimefanyika Wilaya za Kilombero na Bagamoyo, ambapo kipato cha mkulima kimepanda kutoka tani sita hadi 11 kwa ekari moja.

"Nataka niwaambie jambo moja wenzenu kati ya maeneo niliyotaja wameanza kunufaika kwa sababu hawana tena tatizo la soko kwa sababu wawekezaji wakubwa wananunua mazao yao kwa bei nzuri," alisisitiza.

Kwa upande wa Mkurugenzi wa Mamlaka ya Usimamizi na Uendelezaji wa Bonde la Rufiji (Rubada), Aloyce Masanja, alisema mradi huo ambao unasimamiwa na mamlaka yake, upo katika hatua nzuri na wakati wowote utaanza utekelezaji wake. Alisema eneo hilo lina ukubwa wa hekta 44,000 lakini serikali imeamua kulitumia kwa kufuata vigezo vinavyokubalika vya utunzaji wa mazingira.

"Kabla hatujaanza, mkulima wa kawaida alipata kiasi cha debe tano kwa ekari moja, nia yetu watoke hapo na kufikia tani sita kwa mwaka," alisema Masanja.

Diwani wa kata hiyo, Kassim Mnongane, aliishukuru serikali kwa kuwapelekea mradi wa aina hiyo ambao utasaidia ukuaji wa kasi wa maendeleo katika vijiji husika.

Alisema mpaka sasa wamekuwa wakishirikishwa kwa kiasi cha kutosha kwa kila hatua.

Mnongane alitaja changamoto zinazowakabili kuwa ni upotoshwaji unaofanywa na taasisi zisizo za serikali kwa kuwashawishi wananchi kutoukubali mradi

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe