Dk. Mwaka: Matatizo ya mfumo wa uzazi huyumbisha ndoa nyingi
Kuongezeka kwa matatizo ya uzazi kwa familia, ni moja ya sababu
zilizochangiwa kuyumba kwa ndoa nyingi ama kupotea kwa matumaini ya
kupata watoto.
Akizungumza na NIPASHE Jumamosi, Dk. Juma Mwaka ambaye ni mtaalam na
mkurugenzi wa afya katika kliniki ya Foreplan Bungoni jijini Dar es
Salaam, alisema baadhi ya matatizo hayo yamechangiwa na ukosefu wa vifaa
vya uzazi katika hospitali mbalimbali nchini.
Dk. Mwaka alisema kijiografia matatizo hayo yamesababisha Watanzania
wengi wenye matatizo ya kutopata watoto katika ndoa kutafuta njia
mbadala.
Kwa mujibu wa Dk. Mwaka, alisema kliniki yake ina takwimu za 2012 ambazo
wagonjwa waliofika kupatiwa matibabu wakikabiliwa na matatizo ya uzazi
ni 158,954, wengi wao wakiwa wanawake huku wanaume wakiwa wachache
kutokana na waoga.
“Hospitali nyingi hazina vifaa vya uchunguzi wa kina wa mfumo wa uzazi,
kutokana na adha hiyo zimeamini baadhi ya vipimo vya kisasa kama kipimo
cha X Ray, Utrasound ambavyo bado vinaonekana wazi havina uweo wa
kubaini ukubwa wa tatizo,”s alisema Dk. Mwaka.
Alisema katika kupanua wigo wa tiba kwa Watanzania kwa mwaka 2012 hadi
sasa ameshafanya ziara katika mkoa wa Mbeya, Mwanza, Arusha, Dodoma
pamoja na Iringa.
0 comments:
Post a Comment