
Wasanii wa uigizaji, waimbaji na wengine
wameuchangamkia Uchaguzi Mkuu wa mwaka huu wa 2015 na baadhi yao
wamepenya kwenye kura za maoni na wengine kwenda na maji baada ya
kukatwa.
Irene Uwoya alifanikiwa kupenya kupitia CCM viti
Maalumu Vijana Mkoa wa Tabora, Mohammed Mwikongi ‘Frank’ yeye amepeta
kupitia ACT, Joseph Haule ‘Prof Jay’ na Afande Sele wamepenya mkoani
Morogoro kupitia vyama vya Chadema na ACT, Keysher, Said Fella walipeta
kupitia CCM.
Fella alikuwa akiwania udiwani, wakati Keysher alipenya kwenye ubunge viti maalumu walemavu mjini Dodoma.
Wema Sepetu, Wastara Juma, Steven Mengele ‘Steve
Nyerere’, Juma Chikoka ‘Chopa Mchopanga’ ni baadhi ya waliopigwa chini
kupitia chama cha CCM, Rashid Mwinshehe ‘Kingwendu’ yeye bado
haijafahamika kama kapenya kupitia CUF au la.
Sugu
Safari hii kumekuwa na mwamko mkubwa kwa baadhi ya
wasanii kujitokeza kujaribu bahati zao ikiwa ni mara ya kwanza kwa
wasanii wa filamu kuchukua uamuzi mzito kuomba ridhaa kwa raia, watu wa
muziki wao tayari wapo Bungeni.
Joseph Mbilinyi ‘Sugu’, Vicky Kamata, Martha Mlata
ni baadhi ya wasanii wa muziki waliofungua pazia la wasanii kutwaa viti
vya ubunge tangu walipojitosa katika uchaguzi uliopita.
Kabla ya hapo alikuwapo marehemu Kapteni John
Komba na kushinda kwa Sugu kunaelezwa kama ndiyo sababu iliyowaamsha
wengine, kwani walihisi kumbe kila kitu kinawezekana kwa kuwa
haikutarajiwa kama Sugu angepita kupitia upinzani na safari hii
ameteuliwa tena kutetea nafasi yake.
Mwaka huu, wasanii wa filamu ‘Bongo Movie’
waliamua kujaribu bahati zao na kujitokeza kuomba ridhaa ya kuwa wabunge
kupitia vyama va kisiasa huku wasanii wengi wakiomba kupitia CCM na
wawili tu wakiomba kupitia vyama vya upinzani.
Frank ameomba ridhaa ya kupeperusha bendera
kupitia chama kipya cha ACT na anagombea jimbo la Segerea, huku
mchekeshaji Kingwendu’akigombea jimbo la Kisarawe kwa tiketi ya Chama
cha Wananchi (CUF).
Walioomba kupitia CCM walikuwa ni wengi na kura
hazikutosha hivyo walishindwa na wakongwe wa chama hicho na kufanya watu
waamini kuwa kupata nafasi ndani ya chama hicho si kazi rahisi, pamoja
na wasanii kuwa na mvuto katika kukusanya watu, ila suala la kura za
maoni ni changamoto.
0 comments:
Post a Comment