
Mugiraneza kutoka APR amesema,
amemtazama Niyonzima wa Yanga ambaye kwenye kikosi cha timu ya taifa ya
Rwanda ‘Amavubi’ ni pacha wake wakicheza kiungo namba 6 na 8 na kuona
amefanikiwa mno kisoka na kimaisha na kuamua kujaribu bahati yake
Tanzania.
Mugiraneza kutoka APR amesema, amemtazama
Niyonzima wa Yanga ambaye kwenye kikosi cha timu ya taifa ya Rwanda
‘Amavubi’ ni pacha wake wakicheza kiungo namba 6 na 8 na kuona
amefanikiwa mno kisoka na kimaisha na kuamua kujaribu bahati yake
Tanzania.
Akizungumza na Mwanaspoti, Mugiraneza ambaye awali
Yanga ilimtaka lakini aliwatolea nje, alisema: “Unajua nimemwangalia
Niyonzima ambaye alikuwa pacha wangu APR na mpaka sasa kwenye timu ya
Taifa, baada ya kuondoka amefanikiwa na anaporudi nyumbani Rwanda
anaheshimika, ndiyo na mimi nikaamua nisifanye mchezo.
“Unajua awali, timu zilinifuata lakini kwa sababu
ya utoto nilikataa, lakini sasa ni mtu mzima hivyo nahitaji changamoto
nyingine ili nifikishe malengo yangu.”
Mugiraneza anatarajiwa kutumiwa na kocha Stewart Hall katika nafasi ya kiungo mkabaji na anamjaribu kwenye beki ya kati.
Mugiraneza amekwenda mbali na kusema, kutokana na mazingira aliyoyaona kwenye kikosi cha Azam, anaamini atatimiza ndoto zake.
“Azam ni timu kubwa, wana kila kitu, kama uwanja mzuri, gym, bwawa na mambo mengine mengi. Nikiwa makini nitafaidika,” alisema.
0 comments:
Post a Comment