Sunday, July 13, 2014

Emmanuel Okwi
MASTRAIKA wa Yanga, raia wa Uganda, Emmanuel Okwi na Hamis Kiiza, wamemfanya kocha Mbrazili Marcio Maximo kushindwa kusajili fowadi mpya.
Okwi na Kiiza bado hawajaripoti kwenye mazoezi ya Maximo na wapo kwenye kambi ya timu ya taifa ya Uganda ‘The Cranes’ inayojiandaa na mechi ya kufuzu fainali za Kombe la Mataifa ya Afrika dhidi ya Mauritania.
Maximo aliliambia Mwanaspoti: “Nimekuwa na mapendekezo mengi ambayo nimepeleka kwa viongozi wa klabu likiwemo la kuleta mastraika wapya, lakini hilo limekwama kwa sasa mpaka pale kina Okwi na Kiiza watakapowasili.
“Wakishawasili nitahitaji kuwafanyia uchunguzi wa umakini ili nibaini iwapo nitahitaji straika mpya au nitajitosheleza nikiwa nao.” Alisisitiza kwamba ana mipango ya kuifanya Yanga kuwa klabu ya kimataifa na ambayo itajitangaza yenyewe ikiwa inaigwa na wengi. “Sitaki kusema kuwa na sisi tunataka kuwa kama klabu za TP Mazembe ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo yenye kusifika kwa utajiri. Sisi Yanga tunataka kuwa kama Yanga kwenye soka la Afrika.
 “Nataka kuiendeleza Yanga nje na ndani ya uwanja kwakuwa wanachofanya viongozi na mashabiki kinahitaji kuifanya Yanga kuwa ya kipekee na ya kimataifa.
“Hisia za watu mitaani zinanifanya niamini kuwa Yanga inatakiwa kuwa ya kiprofesheno, pia Yanga yenye nidhamu ya hali ya juu na pia yenye kuleta ushindani nje na ndani ya nchi.”
Wiki hii Maximo alifanya uamuzi mgumu kwenye kikosi cha Yanga baada ya kuwarejesha kundini Abuu Ubwa na Hamis Thabiti waliokuwa wametemwa kwenye kikosi hicho kwa nyakati tofauti ambapo jana Ijumaa alilitolea ufafanuzi suala hilo.
Maximo alisema: “Nina jukumu la kuwaweka vizuri wale vijana waliokuwa kwenye kikosi cha timu ya Taifa chini ya miaka 17 wakati nikiwa na Taifa Stars ambao kwa sasa wameonekana kupotea na pia wale wanajitahidi kupanda hususani wa timu ya vijana ya Yanga.
“Naamini wachezaji kama kina Thabiti, Ubwa wana nafasi ya kurudisha ubora waliokuwa nao miaka minne iliyopita wakiwa Serengeti Boys (timu ya taifa ya vijana chini ya miaka 17 ). Hii  itaisaidia Yanga kwa siku zijazo. Tayari pia nina wachezaji kama saba wa timu ya vijana.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe