
RIO DE JANEIRO, BRAZIL
KOMBE la Dunia nchini Brazil limefika patamu, lakini mambo ni matamu zaidi Manchester United.
Mageuzi yameshika kasi klabuni hapo baada ya
miamba hao ya Old Trafford kuanza kutumia pesa kufanya usajili wa nyota
wapya watakaorudisha hadhi ya klabu msimu ujao.
Mabingwa hao mara 20 wa Ligi Kuu England wametumia
Pauni 58.8 milioni kuwanasa Luke Shaw na Ander Herrera ikiwa ni mkakati
wa kocha mpya, Louis van Gaal, anayepania kuirudisha kileleni timu hiyo
baada ya mambo kwenda kombo msimu uliopita.
Hadi kufika jana Ijumaa, Man United ilitarajia
kukamilisha uhamisho wa beki wa kushoto, Mwingereza Shaw, ambaye
anawagharimu Pauni 30 milioni, hilo likitokea katika kipindi cha saa 24
baada ya kumnasa kiungo wa Athletici Bilbao, Herrera kwa dau la Pauni
28.8 milioni.
Wakati kocha Van Gaal akiwa na majukumu kwenye
kikosi cha Uholanzi katika fainali za Kombe la Dunia akijiandaa na mechi
za mtoano ambapo kesho Jumapili atamenyana na Mexico, amefurahishwa na
Makamu Mwenyekiti wa Man United, Ed Woodward kwa kufanya usajili huo
huku ikitarajia kuwanasa mastaa wengine.
0 comments:
Post a Comment