Thursday, June 12, 2014

Wastara (katikati) akibadilishana mawazo na msanii mwenzake Denis Swea ‘Dino’ (kulia) na mdau mwingine ambaye hakutambulika jina.
Wastara akiwa katika kazi ya kuosha mojawapo ya magari.Muonekano wa Car wash ulivyo.Wadau mbalimbali waliojitokeza kwenye uzinduzi huo.Hapa wakipata chakula.
(Picha/habari: Gladness Mallya na Hamida Hassan/GPL)
Stori:Na Gladness Mallya na Hamida Hassan
MSANII wa filamu Bongo, Wastara Juma, ameamua kutoka kivingine tofauti na filamu ambapo amefungua sehemu ya kuoshea magari ‘Car wash’ inayojulikana kwa jina la Mamii White ikiwa ni njia mojawapo ya kuendelea kujiongezea kipato.
Wastara amezindua Car wash hiyo iliyopo maeneo ya Tabata Muslim jijini Dar es Salaam ambapo watu kibao wamehudhuria na magari yao huku wakipewa ofa ya kuoshewa na kusherehekea kwa kula na kunywa na kucheza muziki.

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe