ILIPOISHIA
Siku ziliendelea kukatika, Annabel alizidi kumpenda zaidi mtu ambaye wala hakuwa na mapenzi yoyote yale moyoni mwake juu yake. Huku moyo wake ukiendelea kujilazimisha kumpenda Annabel, hapo ndipo alipompata msichana aliyeona kwamba alistahili kuwa mpenzi wake, huyu alikuwa Pamela.
SASA ENDELEA...
Annabel hakujua kitu chochote kile, hakujua kama mtu ambaye alikuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati alikuwa katika mapenzi na msichana mwingine. Kila siku alijitahidi kumuoneshea Jonathan mapenzi ya dhati lakini mvulana huyo hakuwa na shida naye.
Tattoo yenye jina la Jonathan aliyojichora kifuani mwake ilikuwa ni alama moja muhimu ya kumuoneshea mvulana huyo kwamba alikuwa akimpenda kupita kawaida. Wavulana waliokuwa wakimtaka Annabel kimapenzi hawakuwa na nafasi tena, msichana huyo mrembo tayari alikuwa amechukuliwa na mvulana mwingine.
Annabel hakusitisha malezi yake kwa Jonathan, kila siku alikuwa akiendelea kumhudumia lakini akili ya mvulana huyo haikuwa kwake kabisa. Bado Jonathan aliendelea kumtumia msichana huyo kama chemchemi yake ya kuchota fedha kitu ambacho alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Siku ya kwanza ambayo Jonathan alimwambia Pamela kwamba alikuwa akimpenda, msichana huyo mwenye shepu kubwa na macho yaliyolegea hakuwa na kipingamizi japokuwa alifahamu fika kwamba mvulana huyo alikuwa katika uhusiano na msichana kutoka katika shule ya wasichana ya Kisutu, Annabel.
“Simtaki, si mzuri kama wewe,” alisema Jonathan, muda huo alikuwa na Pamela huku akijaribu kurusha ndoano yake.
“Acha kunitania Jonathan, Annabel utamfananisha na kinyago mimi?” aliuliza Pamela huku akitoa tabasamu pana lililoendelea kummaliza Jonathan.
“Nani Kinyago? Wewe? Hapana, u mrembo mno na si kama yeye. Hebu mwangalie Annabel halafu jiangalie na wewe, hakufikii hata robo,” alisema Jonathan.
Maneno yaliyojaa sifa ambayo alikuwa akiambiwa yakaonekana kumfurahisha Pamela, kila alipokuwa akijiangalia, kweli alijijengea sifa na kujiona kuwa msichana mrembo zaidi ya alivyokuwa Annabel.
Hakuwa na pingamizi, sifa zile alizopewa zikamfanya kumpenda Jonathan kwa kuona kwamba kila siku angeendelea kuzisikia masikioni mwake kutoka kwa mvulana huyo.
Mahusiano ya siri baina ya watu hao yakaanza rasmi, hiyo ikawa furaha kwa Jonathan ambaye kila alipokuwa akimwangalia Pamela, alionekana msichana mrembo asiyekuwa na dosari hata kidogo.
Kwa sababu moyo wake ulikuwa umekwishajiwekea kwamba alikuwa akitaka kumlia Annabel fedha ake tu, hakumuonyesha mabadiliko yoyote yale, alijifanya anampenda huku moyoni mwake akimzomea.
Moyo ulitunza siri ambayo kamwe Annabel hakuwa akiifahamu kabisa. Kila alipokuwa akibusiwa, alijihisi kuwa katika ulimwengu mwingine kabisa wenye raha ambao ulimfanya kusisimka. Hakujua kwamba kila kitu kilichokuwa kikitokea kilikuwa unafiki mkubwa.
“Unanipenda?” aliuliza Annabel huku akimwangalia Jonathan usoni.
“Ninakupenda malaika wangu, ninakufananisha na ua zuri litoalo harufu nzuri na yenye kunukia huku mimi nikiwa nyuki mwenye uchu wa kukufuata kwa ajili ya kuchukua vitu muhimu kwa ajili ya kutengeneza asali yangu,” alisema Jonathan.
“Nakupenda pia mpenzi,” alisema Annabel.
“Huwa ninajiuliza, umeumbwa wakati gani, ni mchana au usiku? Kama ni mchana, natumaini Mungu aliacha kazi zake zote kwa ajili ya kukuumba wewe, na kama alikuumba usiku, natumaini alikesha kwa ajili yako tu,” Jonathan alisema maneno yaliyomfanya Annabel kujisikia vizuri, hakujua kama Jonathan alikuwa muigizaji mzuri zaidi ya JB.
Siku ziliendelea kukatika, Annabel alizidi kumpenda zaidi mtu ambaye wala hakuwa na mapenzi yoyote yale moyoni mwake juu yake. Huku moyo wake ukiendelea kujilazimisha kumpenda Annabel, hapo ndipo alipompata msichana aliyeona kwamba alistahili kuwa mpenzi wake, huyu alikuwa Pamela.
SASA ENDELEA...
Annabel hakujua kitu chochote kile, hakujua kama mtu ambaye alikuwa akimpenda kwa mapenzi ya dhati alikuwa katika mapenzi na msichana mwingine. Kila siku alijitahidi kumuoneshea Jonathan mapenzi ya dhati lakini mvulana huyo hakuwa na shida naye.
Tattoo yenye jina la Jonathan aliyojichora kifuani mwake ilikuwa ni alama moja muhimu ya kumuoneshea mvulana huyo kwamba alikuwa akimpenda kupita kawaida. Wavulana waliokuwa wakimtaka Annabel kimapenzi hawakuwa na nafasi tena, msichana huyo mrembo tayari alikuwa amechukuliwa na mvulana mwingine.
Annabel hakusitisha malezi yake kwa Jonathan, kila siku alikuwa akiendelea kumhudumia lakini akili ya mvulana huyo haikuwa kwake kabisa. Bado Jonathan aliendelea kumtumia msichana huyo kama chemchemi yake ya kuchota fedha kitu ambacho alifanikiwa kwa kiasi kikubwa sana.
Siku ya kwanza ambayo Jonathan alimwambia Pamela kwamba alikuwa akimpenda, msichana huyo mwenye shepu kubwa na macho yaliyolegea hakuwa na kipingamizi japokuwa alifahamu fika kwamba mvulana huyo alikuwa katika uhusiano na msichana kutoka katika shule ya wasichana ya Kisutu, Annabel.
“Simtaki, si mzuri kama wewe,” alisema Jonathan, muda huo alikuwa na Pamela huku akijaribu kurusha ndoano yake.
“Acha kunitania Jonathan, Annabel utamfananisha na kinyago mimi?” aliuliza Pamela huku akitoa tabasamu pana lililoendelea kummaliza Jonathan.
“Nani Kinyago? Wewe? Hapana, u mrembo mno na si kama yeye. Hebu mwangalie Annabel halafu jiangalie na wewe, hakufikii hata robo,” alisema Jonathan.
Maneno yaliyojaa sifa ambayo alikuwa akiambiwa yakaonekana kumfurahisha Pamela, kila alipokuwa akijiangalia, kweli alijijengea sifa na kujiona kuwa msichana mrembo zaidi ya alivyokuwa Annabel.
Hakuwa na pingamizi, sifa zile alizopewa zikamfanya kumpenda Jonathan kwa kuona kwamba kila siku angeendelea kuzisikia masikioni mwake kutoka kwa mvulana huyo.
Mahusiano ya siri baina ya watu hao yakaanza rasmi, hiyo ikawa furaha kwa Jonathan ambaye kila alipokuwa akimwangalia Pamela, alionekana msichana mrembo asiyekuwa na dosari hata kidogo.
Kwa sababu moyo wake ulikuwa umekwishajiwekea kwamba alikuwa akitaka kumlia Annabel fedha ake tu, hakumuonyesha mabadiliko yoyote yale, alijifanya anampenda huku moyoni mwake akimzomea.
Moyo ulitunza siri ambayo kamwe Annabel hakuwa akiifahamu kabisa. Kila alipokuwa akibusiwa, alijihisi kuwa katika ulimwengu mwingine kabisa wenye raha ambao ulimfanya kusisimka. Hakujua kwamba kila kitu kilichokuwa kikitokea kilikuwa unafiki mkubwa.
“Unanipenda?” aliuliza Annabel huku akimwangalia Jonathan usoni.
“Ninakupenda malaika wangu, ninakufananisha na ua zuri litoalo harufu nzuri na yenye kunukia huku mimi nikiwa nyuki mwenye uchu wa kukufuata kwa ajili ya kuchukua vitu muhimu kwa ajili ya kutengeneza asali yangu,” alisema Jonathan.
“Nakupenda pia mpenzi,” alisema Annabel.
“Huwa ninajiuliza, umeumbwa wakati gani, ni mchana au usiku? Kama ni mchana, natumaini Mungu aliacha kazi zake zote kwa ajili ya kukuumba wewe, na kama alikuumba usiku, natumaini alikesha kwa ajili yako tu,” Jonathan alisema maneno yaliyomfanya Annabel kujisikia vizuri, hakujua kama Jonathan alikuwa muigizaji mzuri zaidi ya JB.
0 comments:
Post a Comment