Friday, June 20, 2014



KOMEDIANI maarufu Bongo, Haji Salum ‘Mboto’ alijikuta akipagawishwa vilivyo na shoo ya Malkia wa Taarab Bongo, Khadija Kopa kiasi cha kushindwa kujizuia na kupanda jukwaani kuungana na wacheza shoo wake.

Komedian maarufu Bongo, Haji Salum ‘Mboto’ akiwa jukwaani mara baada ya kupagawishwa vilivyo na shoo ya Malkia wa Taarab Bongo, Khadija Kopa.
Tukio hilo lilitokea wikiendi iliyopita katika Uwanja wa Jamhuri, Dodoma ambapo kulikuwa na uzinduzi wa video ya Tulinde Utanzania ambapo mastaa wa Bongo na mashabiki kibao walikuwepo.
...Haji Salum ‘Mboto’ akizidi kutoa sapoti jukwaani katika shoo ya Khadija Kopa.
Mboto akiwa jukwaani alishangiliwa sana, aliposhuka aliwekwa kati na gazeti hili ambapo alisema: “Namkubali sana Khadija Kopa, kiukweli nilivutiwa na kipande alichoimba kwenye wimbo wa Tulinde Utanzania, ndiyo maana sikuona haja ya kujivunga.”

0 comments:

Post a Comment

Designed by Adamu Mwanakatwe